Wednesday, September 17, 2008

DO YOU KNOW CANADIAN CITIZENSHIP ARE NOW EASIER FOR YOU

Foreign students and young professional from Tanzania with the aim to make a living in Canada will probably rub hands with glee as the Canadian government has lessned the conditions for acquiring citizenship.
The new system called CANADIAN EXPERIENCE CLASS will make it increasingly easy for certain temporary foreign workers and foreign students to become permanent residents........
more to come very soon................
Francis

14 comments:

Anonymous said...

lete link

Anonymous said...

vijana mbona uzalendo na nchi hamna

Anonymous said...

uzalendo ukishiba, jua kali wacha wachakarike. We uliyeshiba endelea na uzalendo. watakuunga mkono sahani ikiisha.

Anonymous said...

Acha kudanganya watu kirahisi rahisi hivi.
Hao jamaa wa Canada wana masharti makubwa sana kiasi kwamba process nzima inachukua hata miaka mitatu mpaka minne hivi. Na yote ni Points systems. Ambazo waTZ wengi sisi huku sio rahisi kuwa nazo.
Kuna mitihani ya kiingereza lazima ufanye , haipo hapa TZ na hufanyika kila bada ya miezi mitatu Kenya na South Afrika . Kuna fedha za kuombea hiyo process nzima karibu $2000 na hazirudishwi, ukishindwa Interview. Kuna kushinda interview na kuwa na kiasi cha Millioni kama kumi na mbili hivi Bank yako hivi kwa kipidi kisichopungua miezi mitatu hivi. Then ndo kuna upimaji na Kadhalika.Tatu kuna kukamilikisha kila kitu , then unaenda kufanya kazi kama ulikuwa huna , ukaitafute na sehemu zenyewew ni zile za baridi chachali,au za malipo kiasi kidogo sana. Quebec ni wabaguzi sana wafaransa-wazungu wa kanada wa pale. Wao kifaransa ndo zaidi na huona noma kama mtu uliyekuja ni mweusi.
Sawa jitahidini , lakini pa kwenda sasa kirahisi kiasi ni Newzealand na Australia.
Newzealand ndo mambo mswano.

Lakini mpaka ushinde hivyo vyote na kutimiza points ili uhojiwe ni muda mkubwa sana.
Kwa kuongea ni rahisi sana , lakini kwa kufuatilia sio mchezo.

Anonymous said...

Acha kudanganya watu kirahisi rahisi hivi.
Hao jamaa wa Canada wana masharti makubwa sana kiasi kwamba process nzima inachukua hata miaka mitatu mpaka minne hivi. Na yote ni Points systems. Ambazo waTZ wengi sisi huku sio rahisi kuwa nazo.
Kuna mitihani ya kiingereza lazima ufanye , haipo hapa TZ na hufanyika kila bada ya miezi mitatu Kenya na South Afrika . Kuna fedha za kuombea hiyo process nzima karibu $2000 na hazirudishwi, ukishindwa Interview. Kuna kushinda interview na kuwa na kiasi cha Millioni kama kumi na mbili hivi Bank yako hivi kwa kipidi kisichopungua miezi mitatu hivi. Then ndo kuna upimaji na Kadhalika.Tatu kuna kukamilikisha kila kitu , then unaenda kufanya kazi kama ulikuwa huna , ukaitafute na sehemu zenyewew ni zile za baridi chachali,au za malipo kiasi kidogo sana. Quebec ni wabaguzi sana wafaransa-wazungu wa kanada wa pale. Wao kifaransa ndo zaidi na huona noma kama mtu uliyekuja ni mweusi.
Sawa jitahidini , lakini pa kwenda sasa kirahisi kiasi ni Newzealand na Australia.
Newzealand ndo mambo mswano.

Lakini mpaka ushinde hivyo vyote na kutimiza points ili uhojiwe ni muda mkubwa sana.
Kwa kuongea ni rahisi sana , lakini kwa kufuatilia sio mchezo.

Anonymous said...

Hii, inaonekana inagusa wanafunzi wa kigeni wanaosoma Canada.
Kalagabaho mimi ninayesoma Iringa nitabaki hapa hapa au kwenda Dar-mji mkubwa wa biashara Tanzania nikimaliza chuo. Sina hata uwezo huo wa kwenda huko majuu.

Anonymous said...

nimegundua jambo moja kwamba vijana walioko huko tanzania wanafantasize mambo,na kwa mtindo huu nyie mkikaa na wanigeria mtalia kilasiku.maana hata rom mate wako atakuwa anakuchezea zungu la macho hadi unajikuta umetapeliwa kumbe data zote anazitoa yeye.
angalieni sana vijana mambo siyo rahisi kama mnavyofikiria.
maana hapo home ukiwa na bachelor degree unajiona bonge la msomi,lakini ukitoka nje tu utajigundua we ni kinyoka tu utakapo kuta watu wanadegree 2 au 3 tofauti na wako kwao na hizo kazi unazoziota hawazipati pia.
mambo ya uraia sio rahisi ktk nchi nyingi,process zinakuwa ndefu sana,na mzungu siku zote ujuwe ni mzungu tu,mtakapoishi nao kwao ndipo mtawafahamu.usione kaja kutalii huko na fedha alizosotea kukusanya sasa anatumia ukadhani pia ukiwa huku kwao ndivyo watavyo ku-entertain,wengi hawapendi kabisa uje kuishi kwao maana unaleta gozigozi kwao kwa kujirahisisha kufanya kazi ambazo wanataka walipwe pesa kubwa kwakuwa ni mbaya.
ila jaribuni bahati zenu huenda mkafanikiwa kuwa wakimbizi wa makwenu msikotaka kupendezesha.mnasubiri wengine waje kuwapendezeshea ndipo pa fae kukalika.porojo nyingi za city center,vijideal vivyo na mpango ilimradi utapeli tu.

Anonymous said...

We anon wa September 20, 2008 11:50 PM acha kuweko kona kwa wenzio. Unakuwa hasi saana, acha vijana wapigane kivyao.

Anonymous said...

vijana acha wapigane hajakatazwa mtu,lkn ukweli waelezwe akiamua kuchakarika kajitakia na lolote litalomkuta awe tayari,

isijekua baadae malalamiko kemkem kama wanafunzi walokuepo urusi.

fanya unachofanya likikukuta usijesema hukuambiwa that is the point

Anonymous said...

saahizi mnaona mnakatishwa tamaa kwa kuwa mnaambiwa ukweli.lakini yakikufikeni shingoni kelele zinakuwa nyingi ooh jamani sijui balozi zetu hazitusaidii!ooh mara hiki mara kile. kuweni vidume mkiwa tayari kwa hali zote,ndiyo maana tunao wajalini tunakupeni habari za kweli mapema ili ukiamua kuwa mnyama pori unakuwa tayari unajuwa huko kunasimba pia na nyoka.sio unadhani ni majani tu kula kwenda mbele.mimi yamenikuta sana ndo maana huwa simfichi mtu kitu.na aliye niingiza mjini kwa kunificha alikuwa ni mshikaji wangu.hadi nilipo ingia mkenge ndo akanambia we bwana vumilia tu life ni popote.lakini wakati huo yeye majiyakifika shingo anaagiza majeshi toka home,wakati mie najitoa manundu kivyangu.

Anonymous said...

Ulikosa nauli ya kurudi? Na usifikiri kila mtu anataka kwenda urusi. Mbona matatizo ya wanafunzi wa urusi hayako US au UK?

Unajidai kutoa tahadhari, kaa na tahadhari zako. Hamna tahadhari yoyote wivu tuu umekujaa, "kwa nini na wao?" Wacha tupigene kivyetu.

Anonymous said...

ok go ahead

mtoto akilia wembe mpe.

Anonymous said...

mimi binafsi yamenikuta,kuna jamaa kabla sijaenda uk alinisifia masifa tele mi ntakualika ukifika ntakutafutia kazi nauli yako itarudi na utamake pesa,sjui alifikiri sina uwezo wa kufika huko?

mambo yalipojiseti nkamwambia ntumie hiyo invitation sasa nshapata hela hakunitumia.

mi nkafanya mipango yangu mengine kwa bahati nkafika uk, nkamtafuta anisaidie kupata kazi alikua ananikwepa.

kumbe yeye mwenyewe ni mkimbizi hawezi kumualika mtu yeyote anakwenda kusign solihull kila wiki.

nkagundua kumbe ukienda kwa viza ya visit huwezipata kazi sehemu yoyote ile.maisha yalikua tough kwani vipesa nlokwenda navyo vilinishia kwa bahati nkaongea na mzee bongo akantafutia jamaa alokua na sheria akanibeba,

mwisho nliamua kurudi na kuendelea na masomo nliona ni upuuzi. ushauri nlouapata kwa wengi wa kule nikajiripue msomali underage,
ali npate pa kukaa,ukishakujiripua hamna kusoma college inabidi uwaze kozi za lugha,

ni kujidhalilisha flani,

so kwa wale wanaotaka kwenda uk alimradi yuko uingereza na aende, lkn asitegemee akifika huko maisha yatakua poa na kama ndo kashafika au atapata kujiendeleza na masomo zaidi!ni kujirudisha nyuma kabisa.

hiyo ndio hali halisi

Anonymous said...

Hiyo bwana ni spesho kesi yako usiifanye ni fomula kwa kila mtu.