Wednesday, April 29, 2009

SIKU 100 ZA RAIS OBAMA IKULU!!

Barack Hussein Obama ametimiza siku 100 leo tangu aapishwe kuwa Rais wa Marekani. Wamarekani wana utaratibu wao wa kijadi wa kupima uwezo wa kiuongozi wa viongozi wao wakianza na siku 100 za kwanza. Ni utaratibu wa kihistoria ambao kwa mujibu wao,huwa unaonyesha dalili za jinsi uongozi wa Rais mpya utakavyokuwa. Misingi,misimamo na hulka ya kiongozi wao huonekana ndani ya siku 100! Obama anazidi kujijengea umaarufu na pia kukijengea chama chake cha Democrat umaarufu.Republican wanazidi kubomoka na kuonekana kushindwa katika nguvu za hoja.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali,Barack Obama anazidi kukubalika. Wamarekani wengi wanakiri kwamba anafanya kazi nzuri,ni muwazi na hana zile hulka za kigomvi ambazo marais wengine waliomtangulia walikuwa nazo. Kitendo chake cha kusalimiana na Rais wa Venezuela,Hugo Chavez, hotuba aliyoitoa kule Uturuki,jinsi ambavyo ameanzisha mijadala ya kidiplomasia na nchi kama Iran nk ni baadhi tu ya mifano michache kati ya mingi inayoonyesha Obama ni mtu wa aina gani.Lakini wapo ambao wanasema haeleweki na wala hatabiriki. Bado wafuatiliaji na wakosoaji wa masuala ya kisiasa nchini Marekani wanakuna vichwa vyao kujaribu kumsoma zaidi.

Wakati anaingia madarakani niliwahi kuandika kuhusu tofauti mbalimbali za matarajio ya ulimwengu kwa Obama. Kila mtu alikuwa na bado ana lake.Weusi wengi duniani tunamuona kama kioo au ushahidi kwamba inawezekana na yaliyopita si ndwele bali tugange yajayo.Mashariki ya mbali wanachoomba ni amani.Akiweza kuwaletea amani ya kudumu ni mafanikio ya kutosha.Afrika tunachoomba ni misaada zaidi,kusaidiwa.Tunaamini kwa sababu ni Obama ni “mwanakwetu” basi ni lazima akumbuke alikotoka.

Sasa kama umemfuatilia vizuri Rais Obama utagundua kwamba hajaitamka tamka sana Afrika ndani ya siku 100.Amekuwa akizungumzia zaidi nchi za ulimwengu wa tatu na sio Afrika pekee ingawa nyingi ya nchi hizo zipo barani Afrika.Zaidi aliongelea habari hizi katika mkutano wa G20 huko Uingereza ambapo uwepo wake tu katika mkutano ule ulikuwa ni ishara ya kutosha kwamba huenda yale mabadiliko aliyokuwa anayanadi wakati wa kampeni zake ndio yamewadia. Obama anaonekana kuiangalia dunia kwa mapana zaidi kuliko wengi walivyotarajia.Je hiyo ni kumaanisha kwamba Afrika haipo katika nafasi za juu katika ajenda ya Rais Obama? Sina uhakika.Nampa muda zaidi.Yawezekana ni kutokana na changamoto za hali mbaya ya uchumi wa dunia zinazomkabili. Angalau tunajua hajaacha kumpigia simu “nyanya” ake aliyeko kijijini Kogelo.

Mwisho ni kumpongeza na kumtakia kila la kheri.Akifanya vyema Obama atazidi kuandaa njia ya vizazi vya sasa na vijavyo hususani vya watu weusi.Akichemsha tutaambiwa si mnaona? Tuliwaambia.........

UJUMBE KUTOKA KWA MDAU ANSELM!!

Hello,
Tulifikiri baada ya Test na end of semister examinations kumalizika Mzee utarudi kwa kasi na nguvu tele katika kuindeleza hii blog yetu,lkn tunashangaa kulala kunaendelea,inakuwaje Mkubwa?

Anyway naomba utundike hii kitu kwenye hii blog yetu ili wanajumuiya wapate ujumbe,hii ni katika kuambiana ukweli Kaka,atakayechukia na achukie.

TABIA SUGU ZA WANACHUO
1.Hupenda kwenda baa na kumbi za starehe kuliko Lecture na Semina.
2.Hushinda room kuliko Library.
3.Hufahamu mitindo ya mavazi kuliko Module.
4.Huogopa CARRY,SUP na DISCO kuliko dhambi.
5.Hufahamu waziri wa mikopo kuliko wahadhiri.
6.Huudhulia birthdays,harusi na starehe weekend kuliko Ibada.
7.Hutoa zawadi kubwa kwa boyfriend au girlfriend kuliko kwa yatima na wajane.
8.Hulinda ATM Cards na PENZI kuliko DESA na VITABU.
9.Wapo makini na ratiba ya BOOM kuliko UE.
10.Wanapenda haki ila wanakosa mbinu sahihi ya kuzipigania.

Ni hilo tu kwa leo.
Anselm Mwenda

DUNDULIZA DAR-ES-SALAAM
dundulizanselm@cats-net.com
Tel: +255 22 2126676
Mob: +255 713 238627.

"Samahani wadau kwa kuwa kimya ni vijimambo flani flani vya kukaribia kumaliza shule ndio vinavyochanganya kichwa kwa sasa hivi" William.

IF YOU WANT TO HIDE SOMETHING TO AFRICANS "PUT IT IN THE BOOKS"

Its obviously that it wont be the first time to you to hear that saying,it has been used for so many years as a means of discrediting Africans.

When you try to examine what is real within that phrase of words, you will come up with the conclusion that most of Africans do not like to read the books,but if we knew it we could have ran to libraries to open the books so that we can enjoy the intercourse with superior minds. The president of United States of America Barrack Obama has benefited form the practice of consulting the books and in his witness he said that “I thank the books because they opened my mind”....and I think that is why he is the leading speech maker in the world as most of his speeches has been ranked as the best speeches.

Most of us and especially students in higher learning institutions in Tanzania are somehow narrow minded because of our behaviors of not reading the books and we are used to “madesas” given by our tutors and lecturers....and we misses extra knowledges obtained in the books and that is why we fails in making some analyses to some important aspects of life. Also we fails to make relevant references to our arguments in our normal life and we are the same as laymen when it comes to analysis of different life phenomenas.

I here come before you to urge you that books are the best places we can enjoy the pool of knowledges and precious thoughts.

It is chiefly through books that we enjoy intercourse with superior minds. In the best books,great men talk to us,give us their most precious thoughts, and pour their souls into ours. God be thanked for books. They are voices of the distant and the dead, and make us heirs of the spiritual life of past ages. Books are true levelers. They give all who will faithfully use them, the society, the spiritual presence of the best and greatest race.
William Ellery channing

Thursday, April 16, 2009

UDOM GONA BE REAL SOMEDAY!!

Nimeziona form za application za chuo kikuu cha Dodoma hapo jana....nimeiona structure ya kozi zao na nimeipenda mno na kama watakuwa na mipango iliyo thabiti chuo kitakuwa bora sana hapa Afrika mashariki.

Lakini bado nataka ufafanuzi kwa wale wanafunzi mnaosoma pale,je hizi ni siasa tu au ni kweli mnapata elimu bora,je vifaa vinatosha au hamna hata maabara moja??

Siamini kama serikali imezima moto na kufanya kama ilivyoafanya shule za kata,sitamani chuo kiwe community university...yaani kijaze wanafunzi na kozi lakini zikae kisiasa tu...kuna kozi ambazo hamna chuo chochote Tanzania kam vili Bcom entrepreneurship....lakini je waalimu wapo.....vifaa vipo??

Lakini kama kutakuwa na mipango dhahili na walimu wa kutosha wataandaliwa basi chuo kitakuwa kizuri sana na kitaingia kwenye chati Afrika!! Ila pliiiiz politics zisiingilie hicho chuo!!

ONLINE COURSE IN SCIENCE JOURNALISM(FREE)

Online Course in Science Journalism (FREE)

An online course in science journalism that covers major practical and conceptual issues in science journalism has been launched in English, French and Arabic by the World Federation of Science Journalists in close cooperation with SciDev.Net, the London-based Science and Development Network

The course was designed for use by professional journalists, journalism students and teachers. It consists of eight lessons on topics including: how to find and research stories, exposing false claims, how to pitch to an editor, turning crisis reporting to advantage and more.


Each lesson consists of an e-lecture with examples, self-teaching questions, and assignments.


To learn more and to get started, go to http://www.wfsj.org/course/
SOURCE: CLICK HERE MAKULILO Jr, www.makulilo.blogspot.com

MATOKEO YA UCHAGUZI UDOM!!

(Ijumaa-Machi 27,2009) Chuo Kikuu cha DOOMA (Udom) kulikuwa na Uchaguzi Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi (UDOSO).Mchuano mkali ulikuwa ni kwa wagombea wa nafasi ya Rais wa College of Social Sciences and Humanities,nd.Ambrose Maratho na nd.Terri Gilead.

Matokeo kamili ya uchaguzi huo yalikuwa kama ifuatavyo:-Nafasi ya Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu kizima cha Dodoma (UDOSO),Raymond Magambo alishinda kwa kupata kura 2675 huku mpinzani wake David Nyangaka akiambulia kura 1076.Ngazi ya makamu wa Rais wa UDOSO ilinyakuliwa na nd.Milton Isaya kwa kupata kura 1894 huku mpinzani wake Nd.Eliphace akipata kura 1768.Ngazi ya College,matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:- College of Social Sciences and Humanities,aliyeshinda nafasi ya Rais ni nd.Ambrose Maratho aliyepata kura 1257 huku mpinzani wake Nd.Terri Gilead akiambulia kura 790.Nafasi ya Naibu Rais ilichukuliwa na kijana kutoka Zanzibar,Nd.Bakari Ali Khamis kwa jumla ya kura 1282 huku mpinzani wake Bi.Ngungi Rhoda (mwenye asili ya Kenya) akipata kura 759.College of Education,nafasi ya Urais ilinyakuliwa na Nd.Sabhuni Joel kwa kupata kura 905 huku wapinzani wake Nd.Johannes Paul akipata kura 325 na aliyefuatia ni Dunia Salutwe aliyepata kura 200.Nafasi ya Makamu ilinyakuliwa na Bi.Ndelwa Uria na kumshinda vikali mpinzani wake Nd.Msilanga Miyango.

College of Informatics (wazee wa Computer) hakukuwa na upinzani,kwani kila nafasi ilikuwa na mgombea mmoja mmoja tu.Nafasi ya Rais ni Nd.Honorious Amon na Makamu wake ni James Chambo.

(April 3,2009) siku ya ijumaa,viongozi hao wapya wameapishwa na mwanasheria na kamishna wa viapo,akishuhudia makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDO) ,Prof.Idriss kikula na kupewa ridhaa ya kuanza majukumu yao hayo mazito ya kuwatumikia wanachuo wenzao.
SELEMANI TAMBWEBA.PSPA 2nd Year

NEW ECOLOGICAL SCHOLARSHIP.....!!

Introduction
The Voluntary Ecological Year ("Freiwilliges Ökologisches Jahr, FÖJ") is a scheme for young Germans to work for one year in different fields in the environmental sector. Since 2008 the Tanzania Solar Energy Association (TASEA) in Dar es Salaam together with the FÖJ branch in Schleswig-Holstein (a region in Northern Germany), have made it possible for two Tanzanians to take part in this scheme.
This year again, from August 2009 until August 2010, this opportunity will be available for 2 Tanzanian girls to work in Germany with the aim to further cultural exchange and the protection of the environment. If you are interested in experiencing German culture for one year and work in an NGO in the environmental sector in Germany, hesitate no longer and request your information pack and application form!

Further Information
For the year you will be assigned and work together with a young German participant of the programme in the same project. You will:
- Share ideas and learn from each other about your culture- Experience the German way of life- Improve the understanding of Tanzanian culture in Germany- Learn about global environmental, economical and political issues- Rise the environmental awareness of the Germans- Take responsibility for sustainable development- Work in educational and agricultural projects


Before starting the voluntary work you will take part in seminars in cultural preparation and a short introduction into the German language in Tanzania and Germany. During and after your stay you will meet participants of the FÖJ from different countries to share your ideas and experience.. You will live in a host family in the city of Lübeck nearby your working place and live on a small monthly stipend. Travel expenses are covered by the FÖJ Schleswig- Holstein.
Download an exact description of the work and hosting projects here
What is expected from you?


If you apply you should match the following hard criteria:
- Female aged between 18 and 25 years-

Be generally healthy and fit- Fluent knowledge of the English language- Be motivated to learn the German language- Be able to take responsibility and work on your own command
- Be interested in cultural exchange- Have basic environmental knowledge- You must return to Tanzania after the year and share your experiences with other Tanzanians

If you are selected to go to Germany, you would be furthermore expected to contribute a small part of the administrative and preparation costs in Tanzania to TASEA. The amount will be TSH 150,000, which covers only a small part of the costs we spend for your travels to Dar es Salaam, preparation and language courses as well as visa fees. It should be understood as a symbolic gesture emphasising your motivation. Obtaining the money can usually be done by fundraising, and we can give you assistance in this process.

Furthermore, in case you will be selected to go to Germany, you will be expected to obtain an International Passport as soon as possible, as this will be necessary for applying for a visa.
What you can expect from us:


- All travel expenses are paid for you- We help you apply for a visa and cover the fees- You are paid a monthly stipend in Euro- Your accommodation in a host family is provided for you- You will receive preparation and language seminars in Tanzania and Germany
Application


Download your application form here
Download and fill out the application form. Remember to attach a CV and copies of relevant certificates, i.e. your educational achievments, former work experience and any other activities in political or environmental issues. Please note that the application deadline is the 17th of April 2009. All applications received past this date will not be considered.
Send the application either by e-mail to
info@tasea.org with subject: "Application FOJ" or by post to:

TASEAP.O. Box 32643Dar es Salaam-
Or hand it in to our office
-in Dar, NSSF Building, 3rd Floor, Suite No. 3, Ubungo.- Or in Mwanza: TASEA Mwanza branch, CCM building, 4th Floor, Makongoro Road- Or in Arusha: KAKUTE office, Mjiro, Nanenane Ground- Or in Zanzibar: ZASEA, Wireless Kikwajuni, Stone Town


You will receive a reply in roughly 1-2 weeks. If the reply is positive, congratulations! You will be asked to attend an interview together with other hopeful candidates in Dar es Salaam in the 4th week of April. Only two candidates will be able to go to Germany, and the decision will be made roughly 1-2 weeks after the interview. All further steps until your departure in August 2009 will be enclosed to you at that time.

Thank you very much for your interest, we are looking forward to your application! If you have any queries feel free to contact us at any time:
- You can call us: 0776032462 (Mr. Johannes Hahn), or 0754317158 (Ms. Olivia Lyimo), or 022-2451674 (TASEA office landline)- Or E-Mail us at
info@tasea.org