Sunday, August 31, 2014

BLOG IMEFUFUKA RASMI

Habari zenu wadau.......Za masiku tele.Ni mimi kijanacwenu William niliyeanzishaga hii blog kama miaka 6 iliyopita lakini kwa bahati mbaya ikashindwa kuendelea kutokana na changamoto mbali mbali hali ya kiuchumi ilikuwa ni mojawapo.Tulikuwa na vision kubwa kwa wakati ule lakini tulishindwa kutokana na michakato ya maisha na kutokana na kila mtu kusambaratika baada ya kumaliza vyuo.Ila tunamshukuru mungu kwani wote alitufanikisha maishani tuna kazi nzuri na tuna maisha kwa sasa.Ila sitaki vision yetu ife tufufue hoo kitu iwasaidie wanachuo na ikiwezekana yuwakabidhishe huku tukiwaongoza na kuandaa succession plan ili lisitokee tena kama lililotutokea kipindi kile kwani uwezo wa kifedha pia ulikuwa mdogo kuendesha blog.Tafadhali karibuni sana kwa maoni tufanyaje na tumkabidhi nani sisi tubaki kama wadhamini,ntafurahi ndoto yetu ikitimilizwa na wengine japo sisi si wanafunzi tena.Nilibarikiwa kumaliza ile Bcom na sasa ni muajiriwa wa shirika moja la serikali lakini shule bado zinaendelea kwa sasa.Karibuni sana tubadilishane mawazo kuhusu hili.Cheerz


Tuesday, September 8, 2009

Monday, September 7, 2009

MPIGANAJI GERVAS MKILI AFARIKI DUNIA.....

Alikuwa ni katibu wa DARUSO (Dar es Salaam University Students Organization) mwaka 2000/2001 pale mlimani.Ninaamini wapiganaji wa miaka ya mwisho wa tisini na miaka ya mwanzoni mwa elfu mbili watakuwa wanamfahamu kwani walikuwa pamoja wakiendeleza harakati pale juu mlimani.

Amefariki dunia na mazishi yatafanyika huko Kahama mkoa wa Shinyanga(Rest in Peace Brother)

Nadhani mlioko DARUSO kwa sasa ni challenge kwenu kufanya kilicho chema ili mkumbukwe daima kwa mazuri mliyowafanyia wanafunzi wenzenu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam au chuo chochote hapa nyumbani Tanzania kwani tunapitia the same situation.

Mungu ailaze rorho ya mahali pema peponi na apumzike kwa amani.

YOU WILL ALWAYS LIVE WITHIN OUR HEARTS BROTHER!!!!!!!!

I AM SORRY...........I AM BACK.

Hello guys,

Its me once again,your blogger William Jackson...It has been too long you have not received any of my posts!!First of all receive my sincere apology as it was not my intention to leave our loved blog not updated.

It was my last and hectic semester at my recent University as I was about to get done with my Bcom degree so it was so hard for me to bring the updates from me,Exams and job findings was among the reasons that made me to stay quiet for all that time.I hope I have been forgiven, and today I come before you and not as a student but an auditor of a certain company here at down town Dar es Salaam.I would like to say thanks to the lord the almighty for all he has done in my life,I have reached at the top so when i see down where I am coming from its when I realise the power of his mighty hand.

I would also like to say CONGRATULATIONS to all those who have completed their college education just like Anselm and others,and i hope the lord will bless you to find a good job somewhere better,I know when you were entering Universities you had a adream of good life and better days and you will real graduate when you make it out of the streets.For those who are still at school...that is a golden opportunity use it effectively bcoz opportunity comes once in a lifetime...and when it is gone,it is gone forever and you will leave with the fact that you lost it forever if you do not use it wisely,so watch out students!!
So lets join our hands together for the revival of our blog,you are all welcomed and lets share the ideas and updates from wherever you are.

You are all welcome once again.
yours,
William.

Thursday, June 11, 2009

KWELI NIMEAMINI MSEMO KUWA MAPENZI YANAUA!!

Ilikuwa ni siku ya jumamosi tarehe 06 August nikiwa nimetoka kuona onyesho la muziki wa Joh Makini pale mabibo hostel,nikaamua kupitia chakula ili kidogo nipunguze njaa iliyokuwa imenielemea!!
Baada ya kuchukua chakula nikaanza kujikokota kuelekea chumbani kwangu huku mawazo ya kumaliza chuo na mustakabali wa maisha yangu vikiwa vimetawala kichwa changu......mara nikaona kundi la watu kama 20 mbele yangu wakiwa kama wameduwaa huku wakipiga kelele....nikahisi kuna tukio litakuwa limetokea.
Mara nikamsikia mmoja kati ya wale kadamnasi akisema masikini sijui kama yule dada atapona.......!!

Mara nikasikia kuwa kuna kijana amemchoma kisu na ameelekea mitaa ya ukutani tayari kwa kuruka ukuta....nikaona kweli hili jambo ni anuai...nikawahisha chakula chumbani na kurudi haraka eneo la tukio......nikakuta yule kijana akisulubiwa na watu wenye hasira kali....nikahisi ni kisu cha kawaida,basi nikaambiwa nikashuhudie damu ghorofa ya pili...nilipofika tu nikashika kichwa na kujiuliza amechinjwa ng`ombe au binadamu??
Mara nikasikia nyeti kutoka kwa rafiki kuwa dada Bertha hajafika hata Ubungo akawa amekata roho....(RIP)
Nilihuzunika sana na nikatamani nijue nini hasa mkasa wa mwanajamii mwenzetu wa chuo kikuu kufanya unyama huo??Wakati huo muuaji alikuwa katika zahanati ya hostel akiwa amepoteza fahamu huku wanajamii wakiomba wafunguliwe mlango wammalizie......!!

Ndipo nikapata nyeti kuwa......walikuwa ni wapenzi ila penzi lilikuwa limeingia hitilafu...na msichana akasema hamtaki tena bwana msiba kwani anakunywa pombe na kuvuta bangi....ndipo mkuu huyo alipoamua kufanya kitendo hicho cha kinyama.......ilikuwa nia majira ya 3:45 usiku ndipo aliposhika begi lake la kutorokea na kutumia kisu hicho kumchoma maeneo ya tumbo na moyo kwa zaidi ya mara tatu...nilipoangalia yale matonge ya damu na bwawa lile la damu ndipo nilposhindwa kutambua ni unyama wa namna gani.....hakupata nafasi ya kutoroka kwani tulimdhibiti ipasavyo na yuko jela kusubiri hukumu kali aka maximum sentence!!

Ndipo nilipoamnini kuwa kweli mapenzi yanaua.....na sumu ya penzi ukishairamba huponi hata kwa maziwa.
Watch out guys!!
REST IN PEACE SISTER BERTHA MWARABU.......!!

WHAT A FELLOWSHIP!!

Oscar van Leer Fellowship 2009 for Journalists in Mexico, Kenya, India (Orissa), Peru, Colombia, South Africa, Tanzania, Uganda and Caribbean Region
Call for applications

The Bernard van Leer Foundation is pleased to announce the inaugural Oscar van Leer Fellowship. We invite applications from journalists in qualifying countries (Mexico, Kenya, India (Orissa), Peru, Colombia, South Africa, Tanzania, Uganda and Caribbean Region) who have an interest in covering children’s issues.

Three fellowships will be awarded, consisting of high-level professional training in skills related to journalism about early chilhood development and children’s rights. A four-week, expenses-paid professional training course in the Netherlands conducted by the Radio Netherlands Training Centre will be provided to the successful candidates.

This is a great opportunity for young journalists to further their general profesional development and to establish for themselves a particular area of expertise.

About the fellowship
The Bernard van Leer Foundation is an international philanthropic foundation based in The Hague that seeks to improve opportunities for disadvantaged young children. It has a long and respected track record of working internationally on early childhood development and children’s rights.

The Oscar van Leer Fellowship commemorates Oscar van Leer, the son of the foundation’s benefactor. The inaugural fellowship also marks the foundation’s 60th anniversary.

One of the difficulties the foundation encounters is that young children’s issues are often poorly understood in media coverage, if they are covered at all. The aim of the Oscar van Leer Fellowship is to contribute to a gradual improvement in the quality and quantity of media coverage of early childhood issues by training up-and-coming journalists, giving them knowledge and understanding that they will be able to apply as they progress in their journalistic careers.

Who should apply?
The fellowship is intended for ambitious young journalists with an interest in children’s issues. We don’t expect you to be an expert in children’s issues already – that’s why we’re offering training. But we want you to be interested in learning more about the issues faced by disadvantaged young children, and the ways in which media coverage can raise awareness and shape opinions of them.

Applicants must be connected to a reputable media outlet, either as an employee or as a frequently published freelance contributor, and must intend to continue to pursue a career in the media. The fellowship is open to journalists in all forms of media, including print, radio, television and web.

Application procedure
You should send us, by no later than 18 August 2009:

A completed application form
A letter of motivation
Your resumé (please include an indication of the reach of the media outlet/s for which you work, in terms of circulation or audience figures)
One example of your work, which has something to do with the situation of children in your country. This could be a piece of writing, a short film or radio broadcast. It can be something you have had published already, or it can be something you produce especially for the purpose of accompanying this application. We would like to publish on our website the work submitted by shortlisted candidates, so if the work you submit has been published already, please ensure this would not cause copyright issues.
See the "how to apply" page for details of where to send your application and in what format.

Successful candidates will be announced on 01 October 2009, and will be invited to a presentation in The Hague on 11 November 2009. The training will take place in early 2010.

Info source: http://www.bernardvanleer.org

Tuesday, May 26, 2009

SOME MORE BEAUTIFUL PICTURES OF MAKUMIRA!!

Among the beautiful environments of the infamous University of makumira....but it too soon the whole country will recognise this hidden treausure.




This is the main gate of a beautiful University of Makumira as seen from the front view!!

AMONG THE BEAUTIFUL CAMPUSES IN TANZANIA!!


This is the infamous University known as makumira University but believe it or not...it is among the beautiful campuses in the country by this time.

Watch its beautiful sceneries and then you will agree with me...........

They are sending hollas to all other Universities in Tanzania and abroad and you are all welcomed to Makumira university at thye northside of the Country.

Saturday, May 16, 2009

ESSAY COMPETITION.....ESSAY COMPETITION!!!!

INTERNATIONAL TELECOMMUNICATION UNION (ITU) ESSAY COMPETITION!
The Essay Competition is open to current students and recent graduates in
economics, political science, law, literature, telecommunications, computer
science, information systems and related fields between the ages of 20 and
30 years old.



The winners of the 2009 Essay Competition will be offered the opportunity of
a consultancy contract within the ITU Development Sector's ICT Applications
and Cybersecurity Division for three months.
The winners will be given a contribution towards the cost of an economy
class flight from their place of residence. In addition, they will be paid
the sum of CHF 6000 towards living expenses for the duration of the
contract.

Choose one of the following essay topics to enter the Competition:
- Mobiles for Development: Enabling Low-Cost e-Applications for Rural and
Remote Areas (e-Health, e-Government, e-Environment)
- Protecting Children and Youth in the Internet and Mobile Age: Innovative
Technical and Social Solutions
- Connecting the World Responsibly: Empowering Women and Girls Through
Creative Uses of ICTs
- Personal Information Online (internet/mobiles): Responding to User Safety
Concerns

Deadline for applications: 14 June 2009

For more Infor: Open http://www.itu.int/ITU-D/cyb/cybersecurity/competition/index.html

MDAU
MAKULILO, Jr.
www.makulilo.blogspot.com

Monday, May 4, 2009

USOMI UNA MAANA GANI SASA??

Wasomi wengi Tanzania lakini nchi inavyoongozwa ni upuuzi mtupu na wasomi wapo hawafanyi chochote kuwasaidia wananchi wa kawaida waelewe michakato inavyokwenda nchini na jinsi ambavyo kuna maisha bora zaidi lakini hawayapati......wasomi mnafanya nini endapo vyombo vya habari tu vinatumiwa kwa maslahi binafsi...................!!

Kawaida panya wakiwa wengi hawachimbi shimo na nionavyo mimi tungekuwa na wasomi wachache Tanzania ingekuwa chachu ya maendeleo,lakini kwa bahati nzuri wasomi wetu wa sasa ni warembo(Ma miss) na mamodalz.....sina uhakika kama hawa wasomi wanafanya wanachojua au wanajua wanachofanya,wanafikiri wanachofanya au wanafanya wanachojisikia.

Dhana yangu si pingu, nawe una fursa ya kutoa tafakuri,jadili ili tuondokane na UJAUZITO WA MAWAZO NA UVIVU WA KUFIKIRIA.

Wednesday, April 29, 2009

SIKU 100 ZA RAIS OBAMA IKULU!!

Barack Hussein Obama ametimiza siku 100 leo tangu aapishwe kuwa Rais wa Marekani. Wamarekani wana utaratibu wao wa kijadi wa kupima uwezo wa kiuongozi wa viongozi wao wakianza na siku 100 za kwanza. Ni utaratibu wa kihistoria ambao kwa mujibu wao,huwa unaonyesha dalili za jinsi uongozi wa Rais mpya utakavyokuwa. Misingi,misimamo na hulka ya kiongozi wao huonekana ndani ya siku 100! Obama anazidi kujijengea umaarufu na pia kukijengea chama chake cha Democrat umaarufu.Republican wanazidi kubomoka na kuonekana kushindwa katika nguvu za hoja.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali,Barack Obama anazidi kukubalika. Wamarekani wengi wanakiri kwamba anafanya kazi nzuri,ni muwazi na hana zile hulka za kigomvi ambazo marais wengine waliomtangulia walikuwa nazo. Kitendo chake cha kusalimiana na Rais wa Venezuela,Hugo Chavez, hotuba aliyoitoa kule Uturuki,jinsi ambavyo ameanzisha mijadala ya kidiplomasia na nchi kama Iran nk ni baadhi tu ya mifano michache kati ya mingi inayoonyesha Obama ni mtu wa aina gani.Lakini wapo ambao wanasema haeleweki na wala hatabiriki. Bado wafuatiliaji na wakosoaji wa masuala ya kisiasa nchini Marekani wanakuna vichwa vyao kujaribu kumsoma zaidi.

Wakati anaingia madarakani niliwahi kuandika kuhusu tofauti mbalimbali za matarajio ya ulimwengu kwa Obama. Kila mtu alikuwa na bado ana lake.Weusi wengi duniani tunamuona kama kioo au ushahidi kwamba inawezekana na yaliyopita si ndwele bali tugange yajayo.Mashariki ya mbali wanachoomba ni amani.Akiweza kuwaletea amani ya kudumu ni mafanikio ya kutosha.Afrika tunachoomba ni misaada zaidi,kusaidiwa.Tunaamini kwa sababu ni Obama ni “mwanakwetu” basi ni lazima akumbuke alikotoka.

Sasa kama umemfuatilia vizuri Rais Obama utagundua kwamba hajaitamka tamka sana Afrika ndani ya siku 100.Amekuwa akizungumzia zaidi nchi za ulimwengu wa tatu na sio Afrika pekee ingawa nyingi ya nchi hizo zipo barani Afrika.Zaidi aliongelea habari hizi katika mkutano wa G20 huko Uingereza ambapo uwepo wake tu katika mkutano ule ulikuwa ni ishara ya kutosha kwamba huenda yale mabadiliko aliyokuwa anayanadi wakati wa kampeni zake ndio yamewadia. Obama anaonekana kuiangalia dunia kwa mapana zaidi kuliko wengi walivyotarajia.Je hiyo ni kumaanisha kwamba Afrika haipo katika nafasi za juu katika ajenda ya Rais Obama? Sina uhakika.Nampa muda zaidi.Yawezekana ni kutokana na changamoto za hali mbaya ya uchumi wa dunia zinazomkabili. Angalau tunajua hajaacha kumpigia simu “nyanya” ake aliyeko kijijini Kogelo.

Mwisho ni kumpongeza na kumtakia kila la kheri.Akifanya vyema Obama atazidi kuandaa njia ya vizazi vya sasa na vijavyo hususani vya watu weusi.Akichemsha tutaambiwa si mnaona? Tuliwaambia.........

UJUMBE KUTOKA KWA MDAU ANSELM!!

Hello,
Tulifikiri baada ya Test na end of semister examinations kumalizika Mzee utarudi kwa kasi na nguvu tele katika kuindeleza hii blog yetu,lkn tunashangaa kulala kunaendelea,inakuwaje Mkubwa?

Anyway naomba utundike hii kitu kwenye hii blog yetu ili wanajumuiya wapate ujumbe,hii ni katika kuambiana ukweli Kaka,atakayechukia na achukie.

TABIA SUGU ZA WANACHUO
1.Hupenda kwenda baa na kumbi za starehe kuliko Lecture na Semina.
2.Hushinda room kuliko Library.
3.Hufahamu mitindo ya mavazi kuliko Module.
4.Huogopa CARRY,SUP na DISCO kuliko dhambi.
5.Hufahamu waziri wa mikopo kuliko wahadhiri.
6.Huudhulia birthdays,harusi na starehe weekend kuliko Ibada.
7.Hutoa zawadi kubwa kwa boyfriend au girlfriend kuliko kwa yatima na wajane.
8.Hulinda ATM Cards na PENZI kuliko DESA na VITABU.
9.Wapo makini na ratiba ya BOOM kuliko UE.
10.Wanapenda haki ila wanakosa mbinu sahihi ya kuzipigania.

Ni hilo tu kwa leo.
Anselm Mwenda

DUNDULIZA DAR-ES-SALAAM
dundulizanselm@cats-net.com
Tel: +255 22 2126676
Mob: +255 713 238627.

"Samahani wadau kwa kuwa kimya ni vijimambo flani flani vya kukaribia kumaliza shule ndio vinavyochanganya kichwa kwa sasa hivi" William.

IF YOU WANT TO HIDE SOMETHING TO AFRICANS "PUT IT IN THE BOOKS"

Its obviously that it wont be the first time to you to hear that saying,it has been used for so many years as a means of discrediting Africans.

When you try to examine what is real within that phrase of words, you will come up with the conclusion that most of Africans do not like to read the books,but if we knew it we could have ran to libraries to open the books so that we can enjoy the intercourse with superior minds. The president of United States of America Barrack Obama has benefited form the practice of consulting the books and in his witness he said that “I thank the books because they opened my mind”....and I think that is why he is the leading speech maker in the world as most of his speeches has been ranked as the best speeches.

Most of us and especially students in higher learning institutions in Tanzania are somehow narrow minded because of our behaviors of not reading the books and we are used to “madesas” given by our tutors and lecturers....and we misses extra knowledges obtained in the books and that is why we fails in making some analyses to some important aspects of life. Also we fails to make relevant references to our arguments in our normal life and we are the same as laymen when it comes to analysis of different life phenomenas.

I here come before you to urge you that books are the best places we can enjoy the pool of knowledges and precious thoughts.

It is chiefly through books that we enjoy intercourse with superior minds. In the best books,great men talk to us,give us their most precious thoughts, and pour their souls into ours. God be thanked for books. They are voices of the distant and the dead, and make us heirs of the spiritual life of past ages. Books are true levelers. They give all who will faithfully use them, the society, the spiritual presence of the best and greatest race.
William Ellery channing

Thursday, April 16, 2009

UDOM GONA BE REAL SOMEDAY!!

Nimeziona form za application za chuo kikuu cha Dodoma hapo jana....nimeiona structure ya kozi zao na nimeipenda mno na kama watakuwa na mipango iliyo thabiti chuo kitakuwa bora sana hapa Afrika mashariki.

Lakini bado nataka ufafanuzi kwa wale wanafunzi mnaosoma pale,je hizi ni siasa tu au ni kweli mnapata elimu bora,je vifaa vinatosha au hamna hata maabara moja??

Siamini kama serikali imezima moto na kufanya kama ilivyoafanya shule za kata,sitamani chuo kiwe community university...yaani kijaze wanafunzi na kozi lakini zikae kisiasa tu...kuna kozi ambazo hamna chuo chochote Tanzania kam vili Bcom entrepreneurship....lakini je waalimu wapo.....vifaa vipo??

Lakini kama kutakuwa na mipango dhahili na walimu wa kutosha wataandaliwa basi chuo kitakuwa kizuri sana na kitaingia kwenye chati Afrika!! Ila pliiiiz politics zisiingilie hicho chuo!!

ONLINE COURSE IN SCIENCE JOURNALISM(FREE)

Online Course in Science Journalism (FREE)

An online course in science journalism that covers major practical and conceptual issues in science journalism has been launched in English, French and Arabic by the World Federation of Science Journalists in close cooperation with SciDev.Net, the London-based Science and Development Network

The course was designed for use by professional journalists, journalism students and teachers. It consists of eight lessons on topics including: how to find and research stories, exposing false claims, how to pitch to an editor, turning crisis reporting to advantage and more.


Each lesson consists of an e-lecture with examples, self-teaching questions, and assignments.


To learn more and to get started, go to http://www.wfsj.org/course/
SOURCE: CLICK HERE MAKULILO Jr, www.makulilo.blogspot.com

MATOKEO YA UCHAGUZI UDOM!!

(Ijumaa-Machi 27,2009) Chuo Kikuu cha DOOMA (Udom) kulikuwa na Uchaguzi Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi (UDOSO).Mchuano mkali ulikuwa ni kwa wagombea wa nafasi ya Rais wa College of Social Sciences and Humanities,nd.Ambrose Maratho na nd.Terri Gilead.

Matokeo kamili ya uchaguzi huo yalikuwa kama ifuatavyo:-Nafasi ya Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu kizima cha Dodoma (UDOSO),Raymond Magambo alishinda kwa kupata kura 2675 huku mpinzani wake David Nyangaka akiambulia kura 1076.Ngazi ya makamu wa Rais wa UDOSO ilinyakuliwa na nd.Milton Isaya kwa kupata kura 1894 huku mpinzani wake Nd.Eliphace akipata kura 1768.Ngazi ya College,matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:- College of Social Sciences and Humanities,aliyeshinda nafasi ya Rais ni nd.Ambrose Maratho aliyepata kura 1257 huku mpinzani wake Nd.Terri Gilead akiambulia kura 790.Nafasi ya Naibu Rais ilichukuliwa na kijana kutoka Zanzibar,Nd.Bakari Ali Khamis kwa jumla ya kura 1282 huku mpinzani wake Bi.Ngungi Rhoda (mwenye asili ya Kenya) akipata kura 759.College of Education,nafasi ya Urais ilinyakuliwa na Nd.Sabhuni Joel kwa kupata kura 905 huku wapinzani wake Nd.Johannes Paul akipata kura 325 na aliyefuatia ni Dunia Salutwe aliyepata kura 200.Nafasi ya Makamu ilinyakuliwa na Bi.Ndelwa Uria na kumshinda vikali mpinzani wake Nd.Msilanga Miyango.

College of Informatics (wazee wa Computer) hakukuwa na upinzani,kwani kila nafasi ilikuwa na mgombea mmoja mmoja tu.Nafasi ya Rais ni Nd.Honorious Amon na Makamu wake ni James Chambo.

(April 3,2009) siku ya ijumaa,viongozi hao wapya wameapishwa na mwanasheria na kamishna wa viapo,akishuhudia makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDO) ,Prof.Idriss kikula na kupewa ridhaa ya kuanza majukumu yao hayo mazito ya kuwatumikia wanachuo wenzao.
SELEMANI TAMBWEBA.PSPA 2nd Year

NEW ECOLOGICAL SCHOLARSHIP.....!!

Introduction
The Voluntary Ecological Year ("Freiwilliges Ökologisches Jahr, FÖJ") is a scheme for young Germans to work for one year in different fields in the environmental sector. Since 2008 the Tanzania Solar Energy Association (TASEA) in Dar es Salaam together with the FÖJ branch in Schleswig-Holstein (a region in Northern Germany), have made it possible for two Tanzanians to take part in this scheme.
This year again, from August 2009 until August 2010, this opportunity will be available for 2 Tanzanian girls to work in Germany with the aim to further cultural exchange and the protection of the environment. If you are interested in experiencing German culture for one year and work in an NGO in the environmental sector in Germany, hesitate no longer and request your information pack and application form!

Further Information
For the year you will be assigned and work together with a young German participant of the programme in the same project. You will:
- Share ideas and learn from each other about your culture- Experience the German way of life- Improve the understanding of Tanzanian culture in Germany- Learn about global environmental, economical and political issues- Rise the environmental awareness of the Germans- Take responsibility for sustainable development- Work in educational and agricultural projects


Before starting the voluntary work you will take part in seminars in cultural preparation and a short introduction into the German language in Tanzania and Germany. During and after your stay you will meet participants of the FÖJ from different countries to share your ideas and experience.. You will live in a host family in the city of Lübeck nearby your working place and live on a small monthly stipend. Travel expenses are covered by the FÖJ Schleswig- Holstein.
Download an exact description of the work and hosting projects here
What is expected from you?


If you apply you should match the following hard criteria:
- Female aged between 18 and 25 years-

Be generally healthy and fit- Fluent knowledge of the English language- Be motivated to learn the German language- Be able to take responsibility and work on your own command
- Be interested in cultural exchange- Have basic environmental knowledge- You must return to Tanzania after the year and share your experiences with other Tanzanians

If you are selected to go to Germany, you would be furthermore expected to contribute a small part of the administrative and preparation costs in Tanzania to TASEA. The amount will be TSH 150,000, which covers only a small part of the costs we spend for your travels to Dar es Salaam, preparation and language courses as well as visa fees. It should be understood as a symbolic gesture emphasising your motivation. Obtaining the money can usually be done by fundraising, and we can give you assistance in this process.

Furthermore, in case you will be selected to go to Germany, you will be expected to obtain an International Passport as soon as possible, as this will be necessary for applying for a visa.
What you can expect from us:


- All travel expenses are paid for you- We help you apply for a visa and cover the fees- You are paid a monthly stipend in Euro- Your accommodation in a host family is provided for you- You will receive preparation and language seminars in Tanzania and Germany
Application


Download your application form here
Download and fill out the application form. Remember to attach a CV and copies of relevant certificates, i.e. your educational achievments, former work experience and any other activities in political or environmental issues. Please note that the application deadline is the 17th of April 2009. All applications received past this date will not be considered.
Send the application either by e-mail to
info@tasea.org with subject: "Application FOJ" or by post to:

TASEAP.O. Box 32643Dar es Salaam-
Or hand it in to our office
-in Dar, NSSF Building, 3rd Floor, Suite No. 3, Ubungo.- Or in Mwanza: TASEA Mwanza branch, CCM building, 4th Floor, Makongoro Road- Or in Arusha: KAKUTE office, Mjiro, Nanenane Ground- Or in Zanzibar: ZASEA, Wireless Kikwajuni, Stone Town


You will receive a reply in roughly 1-2 weeks. If the reply is positive, congratulations! You will be asked to attend an interview together with other hopeful candidates in Dar es Salaam in the 4th week of April. Only two candidates will be able to go to Germany, and the decision will be made roughly 1-2 weeks after the interview. All further steps until your departure in August 2009 will be enclosed to you at that time.

Thank you very much for your interest, we are looking forward to your application! If you have any queries feel free to contact us at any time:
- You can call us: 0776032462 (Mr. Johannes Hahn), or 0754317158 (Ms. Olivia Lyimo), or 022-2451674 (TASEA office landline)- Or E-Mail us at
info@tasea.org

Tuesday, March 31, 2009

UCHAGUZI UDOM WAPAMBA MOTO!!

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi wa Serikali ya wanafunzi wa Seriklai ya Chuo kIkuu cha Dodoma (UDOSO) Mh.Dennis Mungai ametangaza kuanza rasmi kwa zoezi la kampeni za Uchaguzi.Kampeni hizo zimezinduliwa leo,alhamisi Machi 19,2009 wakati wa semina elekezi kwa wagombea waliopitishwa kugombea nafasi mbalimbali.Katika semina hiyo,Mh.Mungai aliainisha umuhimu wa taratibu nzuri za kampeni na kutaka zoezi zima la kampeni kuwa huru na haki.

Vitu vya msingi alivyoelezea Mh.Mungai kama angalizo kwa wagombea hao ni pamoja na kuepuka kampeni za matusi,kuepusha rushwa katika kampeni,rushwa na kampeni za amani.vitu vingine ni kutoingiliana katika kampeni,kuzingatia maadili pamoja na namna ya kupeleka malalamiko kwa tume,ambapo alisisitiza kupelekwa kwa tume ya uchaguzi zikiwa katika maandishi tena ikiwa imesainiwa.

Katika semina hiyo kwa wagombea Mh.Mungai alitangaza kuanza rasmi kwa kampeni ambapo uchaguzi wa kwanza utafanyika Machi 25,2009 kwa wawakilishi wa skuli (School Representatives) na viongozi wa Makazi (Block leaders).Kwa wagombea wa Uraisi au Mwenyekiti katika ngazi ya Chuo pamoja na Skuli,kura zitapigwa Machi 27,2009 siku ya ijumaa.Akisisitizia kwa wagombea,Mh.Mungai amewaasa kutofanya kampeni chafu,hasa za matusi na kashfa.Alisema, “Tunaomba kampeni ziwe za amani na kunadi sera…………ukingundulika,tunaku-nulfy(tunakuondoa) katika kinyang’anyiro”.

Aidha Mh.Mungai aliwakumbusha kuwa kampeni zote zitakoma saa 4:00 usiku kwa kampeni za vyumbani.Siku ya jumamosi na jumapili Umoja wa wanafunzi wanahabari wa Udom (UDOJA) uliandaa mdahalo kwa wagombea wa nafasi za juuu mbele ya wanafunzi ambapo wagombea wote wa nafasi za juu walionesha umahiri na uwezo wao wa kujibu maswali.Mchakato unaandelea .


Selemani Tambwe(UDOM)

Saturday, March 21, 2009

NISAMEHENI SANA,SITAMANI IWE HIVYO.....!!

Salamu wadau,
Ninaamini munaendelea vizuri na shughuli za ujenzi wa taifa letu Stagnant....!!Linalojengwa lakini halikui kwani naamini tunawajengea taifa watu wachache kwa kujenga familia zao kwa nguvu zetu zilizokuwa dedicated kwa taifa...yaani unafanya kazi au biashara unakatwa kodi ili ujenge taifa,kumbe wachache wanakula portion kubwa ya kodi na kuacha portion ndogo kwa ajili ya taifa...anyway poleni and stand for your rights and for the betterment of our nation.

Nisameheni kwani nimekuwa kimya,sikutaka iwe hivyo bali ni shule ya UDSM ilivyokaa vibaya,kiasi cha kunifanya mdau nipitie cafe kuweka updates,Jumatatu tunaanza University Examinations na last two weeks ilikuwa matest na maassignment ya kufa mtu,m sorry for that.....!!
Wadau na wanafunzi wote wa vyuo vikuu Tanzaia tuendelee ku act intellectually and refraining from any conduct that will bring discredit to ourselves and higher education at all.......Poleni kwa mliopoteza nafasi zenu vyuoni,everything has a reason brothers...so dont give up and keep your head up!!

Kwa wale mnataka kusoma masters..pliz i urge you to apply for masters scholarship because most of them are almost at closure stages...sababu nyingi deadline ni 31st March.....!1
Asanteni sana
Wenu Mdau Mkuu.

MASTERS SCHOLARSHIP FOR YOU!!

Masters Scholarships in Tanzania from Embassy of Belgium & Belgian Technical Cooperation (BTC)
Embassy of Belgium & Belgian Technical Cooperation (BTC)Opportunity for scholarships for Masters studies in TANZANIA Starting in the academic year 2009-2010 The Embassy of Belgium in Dar es Salaam and BTC in collaboration with President’s Office, Public Service Management, announce the availability of a limited number ofscholarships for Master studies in Tanzania for the new academic year 2009-2010.
Applicants must have the Tanzanian nationality and be no more than 40 years of ageon 1st May 2009, have a relevant Bachelor degree.

The requested course must be related to the professional activity of the applicant and he/she must have at least two years of relevant working experience.The requested course must be in line with the priority sectors (Basic Health Care,Education, HIV/AIDS Care and Prevention, Agriculture and Food Security, PublicAdministration, Justice, Environment and Water Management)
which foster therealisation of the Tanzania Vision and MKUKUTA.All applicants must be in the possession of an official admission letter prior tosubmission of the scholarship request.Both applications are open to people from public and private sector as well as civilsociety. Female candidates are strongly encouraged to apply. Applicants need tohave the written approval of their employer.
Standard application forms can be obtained from the President’s Office, PublicService Management,
Division of Human Resource Development
PO Box 2483,
Dares Salaam,
Tel. 2118531-4/2122908,
Fax. 2125299 or on www.estabs.go.tz or
fromthe Embassy of Belgium,
5,
Ocean Road, Dar Es Salaam
(email:daressalaam@diplobel..be) or
from the BTC office,
1271, Haile Selassie Road,
Oysterbay,
Dar Es Salaam
(email: daressalaam@diplobel.be).
Completed andsigned application forms have to be submitted with certified true copies of alleducational certificates.
All applications (Original application file + 1 copy) have to be submitted to thePresident’s Office,
Public Service Management,
Division of Human ResourceDevelopment
P.O. Box 2483, Dar es Salaam.
The deadline for submission is 30thMay 2009.
It is recommended to send a copy of the application file to the Embassy of Belgium,
Ocean Road 5,
P.O. Box 9210 Dar es Salaam.
APPLICATION FORMS: CLICK HERE
SOURCE: CLICK HERE
MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com

Thursday, March 5, 2009

Master`s Scholarship in Climate Change 2009-Dernmark

Denmark offers a number of full scholarships within studies of climate change.Study climate change in Denmark - apply for a COP15 Climate ScholarshipClimate change is one of the major challenges that our world faces today. In December 2009, Denmark will host the United Nations Climate Change Summit. To emphasise the importance of sustainable climate solutions, the Danish government is now launching the ‘COP15 Climate Scholarship’ for highly qualified students.

The scholarships, which cover both tuition fees and living expenses, are made available for a range of excellent two-years Master’s programmes, including MSc programmes in wind energy, environmental engineering or sustainable energy planning.BackgroundIn line with the overall aim of securing a climate friendly Climate Conference, the Danish Government has decided not to give any gifts or conference-kits for COP15 participants. The resources saved is instead used to create the ‘COP15 Climate Scholarship’, which gives a number of international students the opportunity to pursue a masters degree within climate change studies at a university in Denmark.How to applyApplications are made directly to the university.
When you apply for a masters programme, you should indicate your interest in applying for the COP15 Climate Scholarship.
The following master programmes are available under the scholarship programme.

Please note the deadline at the beginning of March 2009.
Further Scholarship Information and Application

SOURCE: CLICK HERE


MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com

WAANDISHI WA HABARI!!

The Dag Hammarskjöld Scholarship Fund for Journalists is now accepting applications from professional journalists from developing countries for its 2009 Fellowship Program. The application deadline is Friday, March 20, 2009.

The Fellowships are available to radio, television, print and web journalists, age 25 to 35, from developing countries who are interested in coming to New York to report on international affairs during the 64th session of the United Nations General Assembly. The Fellowships will begin in mid-September and extend to late November and will include the cost of travel and accommodations in New York, as well as a per diem allowance.
The Fellowship Program is open to journalists who are native to one of the developing countries in Africa, Asia, South America and the Caribbean, and are currently working full-time for a bona fide media organization in a developing nation. Applicants must demonstrate an interest in and commitment to international affairs and to conveying a better understanding of the United Nations to their readers and audiences. They must also have approval from their media organizations to spend up to two months in New York to report from the United Nations. Click
here for full eligibility and documentation requirements and Fellowship application form.

The journalists who are awarded Fellowships are given the incomparable opportunity to observe international diplomatic deliberations at the United Nations, to make professional contacts that will serve them for many years to come, to interact with seasoned journalists from around the world, and to gain a broader perspective and understanding of matters of global concern. Many past Fellows have risen to prominence in their professional and countries.


This is the 48th year the Dag Hammarskjöld Scholarship Fund has sponsored the Fellowship Program for Journalists. The program is administered on a volunteer basis by journalists at the United Nations, who raise money from foundations, corporations and diplomatic missions.

Questions about the program, eligibility and application process can be directed to
info@unjournalismfellowship.org

SOURCE
http://unjournalismfellowship.org/node/468

Thursday, February 19, 2009

MAVAZI YA WANAFUNZI WA VYUO!!

Nadhani wadau mlifuatilia bunge la Dodoma,

Kati ya maswali yaliyoulizwa na wabunge mojawapo ilikuwa ni mavazi ya watoto wa kike na kiume wa vyuo vya Elimu ya ju,hasa hasa walisisitiza mavazi ya watoto wa kike kuwa si ya tamaduni zetu na yamejawa vishawishi vitupu.

Naibu waziri wa Elimu mama Kabaka alijaribu kuwatetea watoto wa kike na akasisitiza hakuna aliyewahi kufeli kisa mavazi yao.....Mimi bado halijanikaa kichwani nikichukulia mfano wa vyuo vya Dar es Salaam ka mfano.Hivi ni kweli ni kitu ambacho cha kawaida kwa mtu kuvaa mavazi ambayo si muda wake au ambayo hayafai wakati wa lecture au shughuli nyingine za chuo!!

Ukirudi katika mzingira ya kawaida tunayotoka katika familia zetu za kiTZ watoto wa kike na wa kiume huvaa kwa heshima kabisa,ila tatizo hutokea pale wanapokanyaga vyuoni na ndipo vituko huanza ili waende na wakati....mimi nahisi ni balaa na kupoteza utamaduni wetu na pia kujenga picha mbaya kwa jamii!!

Mavazi mazuri kama sketi na magauni ya heshima yamekwenda wapi wadada,au ndiyo sare yenu ya vinguo vya kubana na kuvaa nusu uchi, si usomi wal si kwenda na wakati nahisi ni ulimbukeni na kukosa maadili..tabia hutabiriwa kupitia mavazi pia...hii ndio hufanya hata wazinzi wa mitaani kuhisi watoto wa kike wazuri wapo vyuoni, kumbe ni mavazi mabaya huvutia ngono na uzungu tunaouiga hauna faida!!
Chukueni hatua na badilikeni jamani,hii hufanya nyie kuuza utu wenu ili mpate vitu vya thamani na viwalo vya thamani ili mu sustain kwenye competition zenu na fashion shows zenu za vyuoni!!

Monday, February 16, 2009

SCHOLARSHIP NYINGINE WADAU!!

Full-Time MBA in International Business
The School and company sponsors fund scholarships, awarded as a full or partial exemption from MBA tuition fee.

Scholarships are awarded based on merit and on specific requirements indicated by the School or company sponsors. For specific requirements, download specific scholarship information.
Evaluation criteria


Among evaluation criteria preference is given to:
Significant professional experience
proficiency in Foreign languages
Demonstrated managerial skills
TO be considered for scholarships, candidates must:

Complete and send the on-line application or the PDF application form to the MBA in International Business Meet the requirements stated in the scholarship description
Send all relevant documentation indicated in the competition for scholarship Admission to the MBA program is independent from the scholarship process.
When outcomes for MBA admissions are announced, candidates will be informed if they receive a scholarship and the amount.

Deadline:EU Citizens: 20 August, 2009
Non EU: 31 July, 2009
SOURCE: http://www.mib.edu/cms/data/pages/000039.aspx
MAKULILO Jr,www.makulilo.blogspot.com

MASOMO YAMENOGA,WENGINE WAKO LIKIZO,WENGINE HAWAJUI MUSTAKABALI WAO!!

SAlam wadau,
Ninatumaini mu wazima na munaendelea vizuri na shughuli za kila siku,samahani sana kwa kuwa kimya ni kwamba shule ya UDSM imenoga,wametupokea kwa fujo sana ikiwepo matest,maassignment na mavurugu yote.
ila hatuna wasi kwani twamshukuru mungu kwa kurudi chuoni ili tuendelee kulisukumiza gurudumu la maendeleo liende mbele............

Wenzetu wa IFM wako likizo,twawatakia likizo njema marafiki,bila kusahau UDOM sina habari za MZUMBE ila ARDHI nao ndio wameruddi chuoni baada ya kukaa mtaani kwa muda wa miezi ipatayo sita,POLENI sana marafiki na hongereni mlio likizo.

Ila katika vyuo vilivyofungulia baada ya ile crisis ya mgomo kuna watu mpaka leo hawajui mustakabali wao kwani hawajarudishwa vyuoni sababu ya kutolipa ada au kutojaza fomu,kwa wale wa UDSM ambao hawajamalizia ada wameambiwa muda umekwisha warudi septemba kurudia mwaka, na wale ambao hawakujaza fomu wameambiwa wao elimu ya juu waisahau,poleni sana marafiki na laana iwarudie mliosababisha wenzetu wapatao 138 kwa mlimani tu kupoteza sifa za kuwa wanachuo,hasa hasa DARUSO mliopita,ndugu Mchibya, Owawa na Silinde damu za hao watu ziwe juu yenu!!...hawa watu hawastahili kurudishwa kwani kwa mawazo yangu ndio waliotupotezea marafiki zetu!! ufinyu wa mawazo yao ndio uliosababisha yote haya,athari nyingine walioileta ni kufutwa kwa mazoezi kwa vitendo kwa mwaka huu,yaani field....zitafanyika next year!!


mungu tubariki wanavyuo wote Tanzania......tupe hekima na tusaidie kutatua matatizo yetu kisomi,na tusaidie tulete mabadiliko nchini.....marafiki mliopotea poleni ila mungu hamtupi mja wake!!

Tuesday, January 20, 2009

SIDHANI KAMA WATASOMA VIZURI....SINA UHAKIKA!!

Salamu Wadau
Samahani kwanza kwa kutoonekana kwa muda mrefu wala kutopata updates kwa muda mrefu!!
Ila ninafahmu wengi wenu mnaelewa kilichokuwa kinaedelea na hamtanilaumu kwani nilikuwa katika kipindi kigum mdau wenu,kipindi hicho kigumu kimesababishwa na viongozi wa chuo changu na wanaharakati feki kwa kuanzaisha migomo wasiyojua itatupeleka wapi.....kwani mpaka leo hii ninavyoongea mdauu wenu jina langu halijatoka na sijasajiliwa na masharti yote nimetimiza ila kwa mbinde.....!!

Nimepitia uzoefu flani mgumu katika maisha yangu ya elimu,uzoefu wa kugombana na chuo na serikali....na mwishowe nime concede defeat kwani chuo na serikali ndio vimepata ushindi na wenzetu wengi bado wako nyumbani hawajui hatma yao!!mungu wasaidie kwa sababu sio kosa lao kosa ni la siasa ilivyoingia vyuoni na viongozi wa wanafunzi wabovu na wanaharakati feki wasiotumia hoja na usomi bali nguvu!!wanafunzi wapatao 2000 inasemekana wamefutiwa udahili japo bado sijaaminiamini vile,na wengineo masikini wasioweza kulipa ada bado wako nyumbani....laana kwa viongozi mlioandaa mgomo na wanaharakati feki,na nyie chama cha siasa cha CHADEMA muwe makini siku nyingine mkiandaa mgomo,mmetupotezea marafiki wengi,vita vyenu na CCM pelekeni nje ya chuo!!vyama vyote vya siasa tawala na msio tawala tuko chini ya miguu yenu msitupotezee muda wetu wa masomo kama ni haki zetu tunazijua na tutaidai wenyewe hatutaki mikono yenu!!

Swali langu ni kwamba fujo zote zilizofanyika na masharti magumu yaliyowekwa na chuo..je wanafunzi watasoma vizuri kweli....maanayake wengi wako affected psycologically.........hata hao endapo chuo kitakuwa na huruma ya kuwarudisha sidhani kama watakuwa kawaida...mungu tusaidie!1Nakuja kwenu chuo kikuu cha Dar Es Salaam....Salamu kwako proffesor mkandala...baba naomba uwarudishe marafiki zetu chuoni,wengi sio kosa lao wanakuwa punished kwa kitu ambacho hawajafanya,kosa ni la wanaharakati feki na wachochezi ambao mimi siwaungi mkono na niko tayari hao wapoteze chuo na sio hao 2000 wasio na hatia,na nina mifano ya baadhi yao ambao hawakugoma kabisa...lakini inaonyesha hawatarudi chuoni...ninaomba uwasamehe mkuu!!
ninaongea haya kwa uchungu sana na ntaongea tena post ijayo!!

waliotimiza masharti ndio hivyo tayari wanarudishwa na wameshapewa vitambulisho vipya na karibia wanaanza masomo!!...mungu wangu wasaidie waliobaki ba wasaidie waanzae masomo vizuri ili wasiathirike na uzoefu mgumu waliopitia....!!...na ninaomba wanafunzi wabishi mpunguze ubishi wenu na tusolve matatizo yetu kisomi!!

Asanteni,Mdau Wenu
William!!

Monday, January 19, 2009

HII SIO ELIMU NI VITA........!!SOMA HAPA;

Viongozi wasisitiza wataandamana kushinikiza wenzao warejeshwe ::
Wapanga kuvaa vitambaa vyeusi kuomboleza msima elimu ya juu ::
Kamanda Kova aonya kama hawana kibali wasithubutu, watakiona cha moto
WANAFUNZI 2,000 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliofutiwa udahili, wameapa kutumia kila mbinu kuhakikisha wanajiunga na wenzao chuoni hap oleo, wakitishia kuwa hata ikibidi wafe, basi wapo tayari. Moja ya mbinu walizopanga kuhakikisha wanafunguliwa lango kuu na kuingia chuoni, ni pamoja na kufanya maanadamano makubwa, yatayowalazimisha walinzi kufungua lango la kuingia chuoni.
Ingawa hawakuomba kibali cha polisi, wanafunzi hao wamesema watafanya maandamano hayo kwa amani, huku wakiwa wamevaa vitambaa vyeusi kuashiria msiba wa elimu ya juu Tanzania.

Mbali na maandamano hayo, baadhi ya viongozi wa wa wanafunzi wa chuo hicho kwa kushirikiana na wenzao kutoka Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba na Afya cha Muhimbili (MUHAS), Umoja wa Vyuo vya Elimu ya Juu vya Umma Tanzania (UVEJUTA), wamesema wapo tayari kumwaga damu. “Kesho (leo) ni siku itakayotumika kumwaga damu za maskini ili kuleta haki katika elimu ya juu Tanzania. Bila haki hakuna amani,” alisema Rais wa Chama cha Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (DARUSO), Anthony Machibya, huku akiungwa mkono na viongozi wenzake ambao jana walikutana kupanga mikakati ya kufanikisha maandamano yao leo.

Aliwataka wanafunzi na wananchi walio jirani na chuo hicho kujitokeza kwa wingi kuwaunga mkono pale watakapoandamana kudai haki zao. Wakati wanafunzi hao wakijiandaa kwa maandamano hayo, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limesema maandamano hayo ni batili na kuwataka viongozi hao wa wanafunzi wasijidanganye kufanya hivyo. “Sisi hatujiandai kwa ajili ya wanafunzi, sisi tuko tayari muda wote kuzuia uhalifu usitokee.

Kama wamesema wanaandamana wafanye hivyo kama wana kibali, vinginevyo watawajibika kwa kitakachotokea kwenye maandamano hayo,” alionya Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova. Kamanda Kova alisisitiza kuwa nchi lazima iendeshwe kwa kufuata sheria na kwamba hakuna mtu mwenye mamlaka ya kuamua anachotaka kufanya, hata kama kinapingana na sheria za nchi.

Kamanda Kova alisisitiza kuwaonya viongozi hao wa wanafunzi akisema kama hawana kibali, wasithubutu kuandamana kwani madhara ya kufanya hivyo wanayajua. Kutokana na matangazo ya chuo hicho, leo wananchi wa kawaida hawataruhusiwa kukanyaga ardhi ya Chuo Kikuu bila kuwa na kibali maalumu, ingawa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wataruhusiwa kuingia ili mradi tu wavae sare za shule zao. Hata hivyo, hadi jana mchana, mabasi yalikuwa yakiendelea kupitia katika eneo la Chuo Kikuu kama kawaida, tofauti na tangazo la chuo hicho lililotangaza kusitishwa kwa utaratibu wa kawaida wa usafiri hadi Januari 23, 2009.

Uongozi wa chuo hicho ulitangaza kuzifunga barabara zote zinazoingia katika chuo hicho ili kupisha usaili na udahili wa wanafunzi wanaorejea chuoni hapo kuanzia leo. Lango lililopo jirani na Chuo cha Maji lilitajwa kuwa litatumika kwa watu wanaoingia chuoni hapo tu na lile lililopo Chuo Kikuu cha Ardhi kuwa litatumiwa na wanaotoka. Wananchi watakaoathirika zaidi na zoezi hilo la siku tano ni wale wanaoishi maeneo hasa, Changanyikeni, Msewe na jeshini ambao njia zinazokwenda huko kupitia Chuo Kikuu zitafungwa. Godbless Charles, ambaye ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa MUHAS, alisema damu itakayomwagika ni ya wanyonge na ndiyo itakayotumika kuikomboa elimu ya juu ya kizazi kijacho. Charles ambaye pia ni Mwenyekiti wa UVEJUTA, alisema hawatanyamazishwa kwa milio ya bunduki, bali wataandamana kwa amani na kama ni vurugu zitaanzishwa na polisi walioandaliwa kuwazuia. Katibu wa Mtandao wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu Tanzania (TSNP) ambaye pia ni Mbunge wa DARUSO, Owawa Stephen, aliwataka wanafunzi kuvaa nguo nyeusi au kufunga vitambaa vyeusi mikononi kuashiria msiba wa elimu ya juu nchini. “Hatutaingia chuoni kwa nguvu, tunachotaka ni haki yetu ya kudahiliwa, maandamano ni ya amani, wakitumia nguvu watupige tu, watawaua labda wawili na hata 10, lakini hatutasita kuidai haki yetu,” alisema huku akiungwa mkono na viongozi wenzake. Wakati wanafunzi hao wakiendelea na msimamo wao huo, menejimenti ya UDSM nayo imeendelea kushikilia msimamo wake wa kuwazuia wanafunzi walioshindwa kujaza fomu wasikanyage eneo la chuo ama sivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Baadhi ya wakazi wanaoishi katika maeneo yanayozunguuka chuo hicho, ambao ili wafike ofisini kwao kwa urahisi, ni lazima wakanyage ardhi ya chuo, wameeleza kusikitishwa kwao na adhabu hiyo, ambayo walidai hawastahili. Jumaa Husein, mkazi wa Changanyikeni, alisema hali hiyo itawaathiri kwani watalazimika kuchelewa kazini kwa kuwa watalazimika kupita njia ndefu na mbovu. Madereva wa daladala zinazofanya safari zake Ubungo-Mwenge kupitia Chuo Kikuu, walisema hawajui wataishi vipi na familia zao katika kipindi cha siku hizo tano za kutopita chuoni hapo. Nacho Chama cha NCCR-Mageuzi kimeitaka Serikali kuchukua hatua za haraka kuhakikisha wanafunzi wote wanarejea chuoni na kuendelea na masomo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Samuel Ruhuza, alisema Serikali imeshindwa kuweka wazi vipaumbele vya taifa katika kuboresha huduma muhimu za jamii. “NCCR-Mageuzi haichukulii kuwa wanafunzi waliotimiza masharti ya kulipa ada kama walivyoelekezwa kuwa ni kigezo cha kuamini kwamba wazazi waoa wana uwezo wa kulipia gharama za elimu ya juu. “Kwa sababu hii, tunaitaka Serikali iachane mara moja na utumiaji wa sera yake mbovu ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu na mikopo, wale wote wenye uwezo wa kufika Chuo Kikuu waweze kupata kile walichokikusudia,” alisema Ruhuza.

Tuesday, January 6, 2009

VYUOTZ IS LIKE NON-ALIGNED MOVEMENT!!

Heri ya mwaka mpya wadau,

Ninaamini wote mko vizuri na tuko tayari kwa ajili ya kuukabili mwaka 2009,ninawashukuru sana kwa kuonyesha sapoti yenu na kuendelea kutoa maoni mbalimbali ni vipi tuiendeshe blog yetu na ipate kuwajumuisha wanafunzi wote wa vyuo ndani na nje ya nchi bila kusahau wale alumni!!
Ningependa kutoa msimamo wetu kuhusu migomo kwani kuna watu katika maoni yao wamesema eti tunatetea upande wa fulani na watu fulani tunawaponda ambacho ni kitu kisicho sahihi.......!!
Post hizo chini tuliweka kwa kutambua athari wanazopata wasiouhusika pindi pande mbili hizo za serikali na viongozi wa wanafunzi wanapohitilafiana.....!!
Nikianza na makosa yanayofanywa na serikali....Kwanza Serikali haiwasikilizi viongozi wa wanafunzi pindi wanapotumia njia za kidiplomasia na kuonyeshwa dharau ya hali ya ju......Pili sera yao mbovu ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu ambazio zinawakandamiza masikini na kuwanufaisha matajiri,kwani huwezi kumpima mtu uwezo wake kwa kutumia makaratasi...Tatu Viongozi wa nchi kutowatembelea wanafunzi vyuoni na kujua matatizo yao na kuwasikiliza katika public talks wala kutobadilishana nao mawazo,wana assume vitu maofisini na kuja na maamuzi mabaya,hasahasa wanapaogopa UDSM mle Nkurumah hall.....Nne na si mwisho...Kutoshirikisha wadau wakuu ambao ni wanafunzi katika utunzi wa sera zinazowaathiri na kuwadanganya kuwa wamefanya utafiti ambao hau apply kwa mazingira ya TZ......!!
Ukija upande wa viongozi wa wanafunzi.....Kwanza Wengi wao hawawezi kutatua matatizo ya wanafunzi na badala yake huyaleta kwa wanafunzi wenyewe wayatatue kwa njia ya migomo.....Pili Wengine hufanya mambo ili kutafuta umaarufu na si kusaidia wanafunzi ili wa gain populatrity itakoyowasaidi kufulfill political interests zao hapo baadaye....Tatu Viongozi wengine wanatumiwa na vyama vya siasa kuchafua chama kingine ili ku fullfill interst za hivyo vyama!! Nne...Wengi wanaoongoza migomo si wale wanaofanya kweli zile kazi za kufuatilia utatuzi wa matatizo ya wanafunzi....yaani hawajawahi kufanya hizo diplomasia wala kufuatilia peacefull....wale ambao wanafuatilia unakuta wanashangaa tu migomo imekwishaanza!!
Hatupingi migomo ila athari zake ndio zinawaumiza wanafunzi ambao wanafukuzwa vyuoni na kurudi vijijini na vilevile kupoteza muda na kufanya vitu ambavyo havikutarajiwa...migomo ni mizuri pale unapofanya demonstration zisizo na athari kubwa kwa majority....si lazima tugoooome mpaka vyuo vifungwe hizo pande mbili zinafaidika lakini wanafunzi wengi innocent wanapata shida....!!
Hivyo kwa mwaka huu 2009 viongozi wa wanafunzi na serikali kuweni makini ili msisababishe athari kubwa kama zilizotokea mwaka 2008!!
Asanteni wadau na endeleeni kuisapoti blog kwa hali na mali!!

KWA WALE WATU WA SHERIA!!

United Nations International Law Fellowship Programme

The 2009 United Nations International Law Fellowship Programme will take place in the Peace Palace in The Hague/Netherlands from 6 July to 14 August 2009.
The 2009 Fellowship Programme will be conducted in English. Fluency in spoken and written English is required. The next Fellowship Programme in French will take place in 2010.
Candidates from the following countries, which were granted fellowships in 2008, are not eligible to apply for a fellowship in 2009:
Botswana, Brazil, China, Ecuador, the Gambia, Ghana, Iran (Islamic Republic of), Malawi, Mexico, Montenegro, Mozambique, Myanmar, Nepal, Saint Lucia and South Africa.
Application deadline: Wednesday, 25 February 2009
Course Content
The Programme comprises participation in seminars, attendance of lectures at

The Hague Academy of International Law,
as well as study visits.
Subjects on the course curriculum may include the following topics:
Law of Treaties, Intellectual Property Law, Law of the Sea, International Protection of Human Rights, Refugee Law, International Criminal Law, International Environmental Law, International Humanitarian Law, International Investment Law, Law of International Watercourses, International Trade Law, Recent Developments in International Law.
Financial Arrangements and Accommodation
The Programme will cover the fellowship recipient’s travel costs in economy class as well as medical insurance, the training material and the registration fee for The Hague Academy of International Law. In accordance with policies and procedures governing the administration of United Nations fellowships, participants will receive a stipend to cover their living expenses. Accommodation will also be provided by the Programme.
Additional places will be made available on a self-financed basis for participants who will have to take care of all the costs associated with their participation (travel, accommodation, living expenses, registration fee for The Hague Academy of International Law).

A more detailed description of previous courses can be viewed

here
.
For additional information, please consult our
"Frequently Asked Questions".
Application forms can be downloaded
here

SOURCE
http://www2.unitar.org/diplomacy/fell_internationallaw_E2.htm

For More Opportunities
MDAU-MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
+13046330978
E-mails
scholarships101@aol.com

makulilo@marshall.edu


SCHOLARSHIPS ZENYE DEADLINE ZA MAPEMA!!

Ndugu wadau,
Kwa ratiba za application kwa ajili ya mwaka wa masomo huu 2009 (mwezi August na September), ndio zinaelekea ukingoni. Hivyo, nimeweka list ya scholarships, hizi zote ni kutoka kwa ERASMUS MUNDUS
http://ec.europa.eu/education/programmes/mundus/projects/index_en.html. Kwa sheria za Mundus, huruhusiwi kufanya application zaidi ya tatu, hivyo chagua upendazo, na unazoona una sifa ndio ujaze, zikizidi tatu, inakula kwako.

Kama muonavyo, list hii kwa pembeni imeonesha DEADLINE yake, hivyo ni mwendo wa faster ktk kufanya application.

LIST
1. Environment
http://www.tu-harburg.de/eciu-gs/pro_joint_jemes.html Deadline 31st Jan 2009

2. Environment Science, Policy and Management
http://www.mespom.eu/node/26 Dedaline 9th Jan, 2009


3. Master in Informatics
http://www.eumi-school.org/edu/eumi/how_to_apply.xml?lang=en Deadline 18th Jan,2009

4. Space Master
http://www.spacemaster.se/index.php?option=com_content&task=view&id=14&Itemid=30 Deadline 15th Jan, 2009

5. Space Technology
http://www.aerospacemasters.org Deadline Febr 2, 2009


6. Security and Mobile Computing
http://www.tkk.fi/Units/CSE/NordSecMob/admission/index.html Deadline 9th Jan, 2009

7. Models and Methods of Quantative Economics
http://www.univ-paris1.fr/rubrique1297.html Deadline 6th Febr, 2009 Also at http://www.univ-paris1.fr/formation/eco_gestion/ufr27/study-in-english/erasmus_mundus/admissions_and_scholarships/article3971.html

8. Sustainable Forest and Nature Management
http://www.sufonama.net/eng/Home/home_7_26.html Deadline 16th Jan 2009
For More Opportunities,
MDAU- MAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
+13046330978
E-mails
scholarships101@aol.com
makulilo@marshall.edu

Tuesday, December 30, 2008

BONOFACE ELPHACE MAGINA,WE SALUTE YOU!!

My stakeholders, Can you accompany me in paying a tribute to the boy named above, Let us acknoweldge his utmost contribution for the betterment of Tanzanians Studying in Russia.....!!

Ni mnamo wiki iliyopita ubalozi wa TZ nchini Urusi umemfukuza nchini humo mwanafunzi huyu na kumrudisha nyumbani TZ.Alikuwa ni Rais wa wanafunzi wa Kitanzaniua wanaosoma Chuo Kikuu Cha Urafiki Lumumba jijini Moscow.

Kisa cha Kumfukuza ni nini??
Kwa sababu ya kufuatilia kwa nguvu zote fedha za wanafunzi wa kitanzania wanazotumiwa na serikali ambazo inasemekana zinaliwa na Ubalozi huo badala ya kuwafikishia wanafunzi!!

Kwa hiyo ubalozi ukaamua kumfukuza na kumkatisha masomo........Serikali mnafanya nini??Pliiiiiz jaribuni kuwa na aibu na kushughulikia swala hilo mwenzetu arudi Chuoni......!!
Huyu ni mpiganaji wa ukweli na mwanaharakati wa Ukweli,Alitrafuta haki ya wenzake peacefully huko Ughaibuni!!

BONIFACE ELPHACE MAGINA WE SALUTE YOU...VIVA OUR TRUE HERO!!

SALAMU KUTOKA KWA MDAU WA DELHI..INDIA.



nawatakia wadau wote wa blog yako x-mass njema na mwaka mpaya.nadhani huu ndio muda wa kujifanyia tathmini wapi tulikotoka na wapi tunaenda,yepi tumefanikiwa na yepi hatukufanikiwa na kuweka strategic intent sawa pae kwenye makosa.


mdau miki kilima from university of delhi,

newdelhi,

india


miki kilima

master of commerce(finance)

department of commerce

delhi school of economics

university f delhi

KWA NINI UDOSO MNAJITENGA NA WENZENU???

UDOSO KUTOJIUNGA NA 'UVEJUTA' NI KOSA KUBWA SANA
Serikali ya wanafunzi wa chuo Kikuu cha Dodoma (UDOSO) imeendeleakufanya madudu mengine kwa kutojiunga na Umoja wa Vyuo vikuu naTaasisi za Elimu ya juu vya Umma Tanzania (UVEJUTA).Alipoulizwa hivikaribuni,Rais wa UDOSO Bw.Joramu Malimia lidai eti kutokushirikishwakatika uanzishwaji wa Umoja huo.Hoja hiyo haina msingi kabisakiuhalisia.
Umoja huo ambao hivi sasa unaundwa na vyuo na taasisimbalimbali za Umma kama vile Chuo Kikuu cha Dar s salaam (UDSM),Chuokikuu kishiriki cha Elimu Dar es salaam (DUCE),Chuo Kikuu kishirikicha Elimu Mkwawa (MUCE,Taasisi ya teknolojia ya Dar Es salla (DIT) navingine umeendesha mgomo wa kupinga Sera mbovu ya Serikali yaUchangiaji wa Elimu ya juu,Ongezeko la Ada pamoja na mambo menginemengi ambayo kimsingi hayaendi vizuri.Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ni Chuo cha Umma,hivyo haikuwa na sibusara kwa uongozi wa UDOSO unaoongozwa na Bw.Malimi kutojiunga naumoja huo.

Viongozi wa UDOSO wanapaswa kujua kwamba kujiunga na Umojahuo si Lazima kushiriki katika kila maamuzi yao ambayo wenyewe wataonahayana msingi.Kwa madai wanayogomea wenzetu hao,ni ya Msingi kabisakwani sisi watoto wa masikini ndio tuanoumia na sera hizi mbovu zaSerikali za uchangiaji wa elimu ya juu.Nina uhakika mkubwa kwamba viongozi wa UDOSO hawakubaliani kabisa nasera mbovu ya uchangiaji wa Elimu ya juu,kama vile Madaraja ya utoajimikopo yasiojali hali za watu,ongezeko kubwa la ada,madaraja ya pesaya Vitendo na mengine mengi.Sasa hiyo hoja ya kutaka mpakamshirikishwe,sijui muandikiwe barua sidhani kama ilikuwa na umuhimuwowote.Kwa kuwa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ni Chuo chaumma,Bw.Malimi na Viongozi wenzie wa UDOSO wakae na watafakari kwakina Umuhimu wa kujiunga na Umoja huo wa Vyuo vikuu vya Umma.Hii nikwa sababu wanaweza kujiunga halafu wakakataa kushiriki katika Mgomohuo unaoendelea kuliko kutojiunga na kutoshiriki katika mgomo huowakati chuo Kikuu cha Dodoma ni Chuo cha Umma na sababu za Mgomo huoni za Msingi kabisa.

Chondechonde UDOSO harakisheni Kujiunga na UmojaHuo mpya wa vyuo vikuu vya Umma (UVEJUTA) ili nasi tuunge nguvu zetudhidi ya Matatizo yanayowakabili Wanafunzi wa vyuo Vikuu vya Ummanchini.

SELEMANI TAMBWE
BA. PSPA
Chuo Kikuu cha Dodoma

HAPPY HOLIDAYS SEASON TOKA KWA MAKULILO Jr,



MAKULILO Jr,

makulilo@marshall.edu
Ndugu wadau,
Napenda kutoa salamu za kipindi hiki cha siku kuu (Holiday Seasons), Heri ya Siku kuu ya Noeli na Mwaka Mpya 2009. Blog ya SCHOLARSHIPS
www.makulilo.blogspot.com inashukuru kwa ushirikiano wa wadau wote hadi kufikia hatua hii (sasa ina miezi 7). Blog inaahidi mambo mengi mazuri, na inatoa wito kwa wadau kufanya applications zaidi khs masuala yetu ya NONDOZI KWA WADAUZI.

Note: Nimeambatanisha na picha yangu, hapo nilikua vekesheni nje ya mjengo wa kaka Barry Obama (WhiteHouse) Washington DC.

MERRY CHRISTMASS & HAPPY NEW YEAR 2009


scholarships101@aol.com
+1 304 633 0978

Wednesday, December 24, 2008

VYUOTZ TEAM TUNASEMA HIVI.........!!

Nimewahi kusikia msemo wa kiingereza unaosema kuwa "good people are good because they ave come to wisdom through failure,we get very little wisdom from success" kwa kiswahili ukimaanisha kuwa watu wema ni wema kwa sababu wamepata hekima kupitia kushindwa kwao,tunapata hekima kidogo sana kupitia mafanikio.

Moja kwa moja ninaekwenda kwenye kusudio la waraka huu kwenu wadau wa vyuotz blogu.kutokana na athari kubwa tulizozipata wanafunzi wa vyuo vikuu na kushindwa kukubwa kwa migomo iliyoandaliwa na viongozi wa wanafunzi na wale wajiitao wanaharakati tumeamua kuungana na kupinga na njia kama hiyo kama utatuzi wa matatizo ya wanafunzi wa vyuo vikuu.

Hebu angalia habari hiyo hapo chini ya gazeti la mwananchi,hizo ni athariwalizozipata dada zetu na wanafunzi wengi wa mikoani walipata shida sana siku wamefukuzwa chuo,na bado athari nyingine nyingi zitaonekana kama zakupoteza muda wetu,kuharibu ratiba za mafunzo kwa vitendo kwa mwaka ujao,chuo kuingia hasara,wanafunzi wa nchi za nje kurudi kwao bila hata semista kuisha na wengine kubaki chuo bila kufanya lolote sababu wenzao hawapo.Kubwa ni dada zetu ambao hata hawakugoma wapo wanauchuma ukimwi kutoka kwa watu ambao siku hizihujulikana kama mafataki!!

Nadhani sasa wanafunzi wengi sasa watakuwa watu wema na watakuwa na maamuzi ya hekima kutokanana kufeli na kushindwa kwa migomo yao,sababu sera hiyohiyowaliyoikataa ndio wamejaza fomu kuikubali,sasa kwanini tuligoma??

Kutokana na kupoteza muda wetu sana,kuharibu ratiba zetu sanana kuharibu malengo yetu sana kutokana na migomo ambayo wanafunzi wengi hawajui siri yake, kwanimingi imeandaliwa na wanasiasa wa vyama fulani na kuwasponse wanafunzi fulani ili waiongoze migomo hiyo na pia kuwaconvice baadhi yaviongozi wa wanafunzi iliwapitishe migomo.....Tulipata kumsikia kiongozi mmoja wa chama cha siasa akisema"Lazima tuwachafue sana chama fulani(jina kapuni)mwaka huu"....alikuwa akiongea wakati wanapanga mgomo huu uliopita....Na siku kabla ya mgomo tukamsikia mwanafunzi mmoja ajiitaye mwanaharakati akimpigia simu kiogozi wa siasa akimwambia "dont worry tommorow you will seeon the media....iliwauma sana wanafunzi wasiopenda migomo.....!!kwani aliisema kauli hiyo akiwa Bar ya maeneo yaleyale ya chuo

Hapa sasa inaonyesha kuwa vyama vya siasa vinatumia vyuo kama "battle ground" yao,hasara tunapata sisi lakini hivyo vyama vya siasa vinaendelea kudumu..tunaingiziwa siasa vyuoni hasara twapata sisi wenyewe kwani wanaharakati hao wamejificha sehemu flaniflani wakiendelea kula mipesa kutoka kwenye vyama vyao.na madai yao wakitimuliwa chuo wanaandaa mgomo wa kuwarudisha!!tunalipinga hilo wana vyuotz......!!
Sasa kama team ya vyuotz na baadhi ya wanafunzi tuliokaa kikao na kutathmini swala hili na athari yake kwa watu wengi na familia za wanafunzi na taifa kwa ujumla tunasema hivi.

(a) Tutaendelea kuzisema athari za migomo na kuwaelimisha wanafunzi watafute njia nyingine za suluhisho la matatizo badala ya migomo.......Na viongozi wa wanafunzi na wanaharakati vyuoni wasiwapotezee muda wanafunzi kwa maslahi yao binafsi na vijihela wanavyopata wakati wanafunzi wengi wanapata shida,dada zetu wameweka rehani miili yao ili waishi mjini na wapate ada za kulipia warudi chuo na wengine wako vijijini wanahangaishana na wazazi kupata hayo malaki ili warudi vyuoni.Lakini wanasiasa walioiandaa tunawaona kila siku mjini kwenye magari yao na hawatusaidii lolote....!!.....Hivyo tunawaomba wadau muisapoti blog yetu iendelee ili tuadress hili tatizo na mengineyo,angalia hapo juu kulia palipoandikwa VOLUNTARY CONTRIBUTION ili ushiriki nasi.

(b) Pili tumeamua kuunda Chama kitakacho adress hilo tatizo la fujo na migomo na tutakisajili kioperate vyuo vyote TZ paler tutakapopata sapotio.Wanafunzi 12 wa vyuo mbalimbali wameonyesha nia na kukaa kikao juzi.majina yao tunayo na ntawapa soon.Profile ya Chamahicho nikamaifuatavyo

Name ofAssociation: Humble Students Against Strikes &Boycots(HSASB)

Motto: There is an alternative best solution instead of strikes and boycotts

Aim: Adressing the effects of boycots & strikes

Mission:To liberate the minds of students so that theycan find other proper means of acquiring their rights.

Vission: Having the secure environment at our Campuses for Study and Life.

Tafakarini Wadau na Chukueni hatua,kama upo tayari kuisapoti nia yetu tunaomba uisapoti blog yetu kuichangia ipate facilities iendelee kuwepo na karibuni watu au mashirika aumawakala mlio tayari mkusapoti chama hicho kiwepo!!Kama uko tayari kusapoti blog fanya hivo Voluntary Contribution kwenye Bank A/c na Kama uko tayari kusapoti Hicho chama tutumie Email Kwenye billjax.nyakua@gmail.com
Vyuotz Team.


Tuesday, December 23, 2008

KWELI ATHARI ZA MIGOMO NI KUBWA....!!

Kutoka gazeti la Mwananchi la leo.

MARA baada ya kutolewa kwa amri ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusimamishwa masomo na kutakiwa kuondoka chuoni mara moja, mambo mawili makuu yaliumiza vichwa vya wanafunzi walio wengi. Mosi watakwenda wapi na pili wataishi vipi ndani ya muda wote chuo kikiwa kimefungwa.Kwa wakazi wa Dar es Salaam, mikoa ya jirani na hata wale wenye jamaa wa karibu mambo haya hayakuwasumbua kwa kuwa walijua nini cha kufanya. Kibarua kilikuwa kwa wale wanaotoka mikoa ya mbali na wakawa hawana kitu mfukoni.Ni mwezi mmoja na ushee sasa tangu kufungwa kwa chuo hicho uchunguzi wa Mwananchi umebaini kuwa baadhi ya wanafunzi wa chuo hicho wameamua kujiingiza katika biashara ya ukahaba kwa kile wanachodai kupambana na ugumu wa maisha unaowakabili baada ya kukosa njia za kurudi makwao.Safari ya gazeti hili kutaka kujua ukweli wa tetesi kuwa baadhi ya wanafunzi waliofukuzwa wanajiuza mitaani zilianzia hosteli ya Mabibo.

Dada mmoja (jina tunalihifadhi) alikuja pale kuomba hifadhi kwa wenzake wanaosoma Taasisi ya Mawasiliano ya Umma na Uandishi wa Habari (IJMC) ambao wao walikataa kugoma.Akizungumza huku akibubujikwa na machozi alisema alikwenda kuwaomba wampe hifadhi baada ya kuchoka na manyanyaso nyumbani kwa mjomba wake aliyekuwa akiishi kwake tangu chuo kilipofungwa. Anamtaja mke wa mjomba wake kama sababu ya kuchukua uamuzi wa kuhama kwa mjomba wake ambaye alikuwa safarini.Huu ndio uliokuwa mwanzo wa kujua kama yapo mambo mengine yanayowasibu wanafunzi wa chuo hiki kikongwe nchini.Nilipomsaili hakusita kusema kuwa kufungwa kwa chuo kumesababisha wanafunzi wengi wa kike kufanya biashara ya kuuza miili yao maeneo mbalimbali ya jiji hasa kumbi za sterehe na burudani."Hamuwezi kuamini nendeni hata hizi baa zilizopo hapa jirani na hosteli utawakuta wanafunzi kama hamuwafahamu mimi nitawaonesha wanajiuza, wanavaa mavazi ya kubana wana weza kununua bia moja au soda kuanzia mchana mpaka jioni wakiwa wanasubiri wanaume, na sio hapa tu hata kule maeneo ya Sinza , makumbusho na Mwenge, kwa kweli hali inatisha sana nyie wenzangu msicheke" alisema kuwaambia wenzake huku akisikitika.Ushabiki wangu wa kutaka kujua zaidi hasa nikitilia maanani hii ilikuwa kazi niliyopewa na mkuu wangu wa kazi nililazimika kumuomba dada huyu twende katika moja ya baa alizozitaja ili nikajionee fahari ya macho.Alikubali na tulijongea baaz ya jirani ambalo naomba kuhifadhi jina lake.Pale niliwakuta akina dada kadhaa alini macho yangu yalituwama kwa mabinti wawili walikouwa wameva nguo fupi huku wakipiga simu na kutoa matusi. Nakumbuka mmoja alikuwa alimaka:‘"inakuwaje mwanume kama huyu atusumbue akili zetu kama angekuwa hana pesa si angesema tusije hapa, shoga nakuomba kuanzia leo usimtafute kama ataamua atakutafuta mwenyewe"Kuanzia hapa nikaanza kupata picha fulani ambayo punde tu ukweli wake ukaja kujidhihirisha baada ya yule dada niliyemuomba kunionyesha hao machangudoa aliponambia maneno yafuatayo:"Kaka umewaona watu wako uliokuwa unawataka ndio hao, hapa ni kidogo tu wewe ukitaka kuwaona wengi nenda Makumbusho ,Mwenge au Sinza kila baa utawakuta wanafunzi, wamesheheni wakiwa wanasubiri wateja wao kama hawa, watoto wadogo lakini ndio hivyo tena.”Baada ya kujionea ya hosteli nilimwomba tena mwenyeji wangu anipeleke eneo la Mwenge kujionea hali ilivyo huko.Hapa nilishuhudia idadi kubwa ya wanawake na magari.

Wanaume walikuja na kuwachagua wanawake kama vile mtu anavyochagua chungwa gengeni."Unamuona yule mwanafunzi yule kashachukuliwa masikini kama angeniona hapa sikui ingekuwaje, lakini ndio ameshaamua jamani yaani hata Jati (jina si rasmi) na yeye anajiuza kweli hali imekuwa mbaya"alisemaKwa kuwa ilikuwa usiku kiasi mwenyeji wangu aliamua kuondoka, nilimshukuru nami nikaamua kwenda kumalizia uchunguzi wangu Makumbusho katika baa moja maarufu eneo hilo . Niliyoyakuta huku ni sawa na ya Mwenge ila hapa kidogo nilipata ugumu kung’amua nani mwanafunzi nani si mwanafunzi. Hata hivyo niliweza kuwabaini baadhi baada ya kuwasikia wakichanganya lugha za Kiswahili na Kiingereza katika mazungumzo yao. Nilihisi walikuwa wanafunzi na ndivyo ilivyokuwa.Niliamua kumfuata mwanadada mmoja aliyekuwa ameketi peke yake, nilimsalimia na kuomba ruhusa ya kujiunga naye katika meza. Nikapata muda wa kurusha ndoano yangu ya kwanza.Sikiliza majibu yake “"Kaka ikiwa unataka kutoka na mimi leo tafadhali nihakikishie kuwa utanipatia elfu kumi kwa usiku mmoja , pia ujue chakula kitakuwa ni juu yako na vinywaji sawa?nadhani umenielewa kaka vinginevyo itakuwa ngumu kaka yangu"Kwa kuwa mimi si mkware na wala sikwenda pale kwa kile ambacho yeye alikifikiri kwa mara ya kwanza nilitaka kuzungumza naye mambo mengine ambayo kwa bahati nzuri alikubali kwa roho moja.

Mwanadada huyo aliyeonekana mdogo kiumri alianza kuniambia kuwa yupo mwaka wa tatu Chuo kikuu cha Dar es Salaam akisomea fani ya sheria, alisema hafanyi biashara hiyo kwa kupenda bali ni kutokana na maisha kuwa magumu“Usione hivi kaka hapa nilipo nipo katika wakati mgumu sana kwani najua ni aibu kufanya hivi lakini, sasa nifanyeje tunakaa chumba kimoja maeneo ya kinondoni tupo watu wanane na wale wenzangu uliowaona wamekaa hapa na kila siku tunatakiwa kula na kufua wewe unafikiria tutatoa wapi hizo pesa" alifafanua sababu ya kufanya uchangudoa.Kwa hali yoyote haya ndiyo matokeo ya kukaidi amri ya chuo na ile ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof. Jumanne Maghembe, iliyowataka kusitisha mgomo na kurudi madarasani wakati wizara ikishughulikia madai yao.Si wote waliogoma lakini mwisho wa siku ilibidi rungu la serikali kuwaangukia waliokuwemo na wasiokuwemo.Inasikitisha.

http://www.mwananchi.co.tz/

JAMANI JAMANI VIONGOZI WA WANAFUNZI HEBU TOENI FIKRA MBOVU VICHWANI KUWA MIGOMO NDIO SULUHISHO LA MATATIZO YETU.

Monday, December 22, 2008

MASTERS BIN NONDOOZ ULAYA MAGHARIBI....!!!

Naomba uweke tangazo hili ktk blog yetu ya jamii watu wapate NONDOZI hapo.Hizi ni Scholarships za ERASMUS MUNDUS

1. Master of Innovation Management
http://www.globalin novationmanageme nt.org/

http://www.globalinnovationmanagement.org/Application_Process.html

2. Master in Strategic Project Management
http://www.mspme.org/

3. Master of Information Technology
http://www.immit.eu/default.htm

4. European Master in Work, Organizational and Personnel Pyschology http://www.uv.es/erasmuswop/

NOTE:
Mkuu hizi zote hazina complications, zote ni za Ulaya ya magharibi, zipo chini ya Erasmus Mundus.


MAKULILO Jr

DAMU YA YOYOTE ATAKEYEPOTEZA CHUO...IWE JUU YENU VIONGOZI WA WANAFUNZI.......!!


Mlipowataka wagome ili mtimize malengo yenu enyi DARUSO na viongozi wa wanafunzi wa SUA,MUCCOBS,ARDHI,DUCE,MUCE na DIT walifanya hivyo pasipo kujua ni nani amepanga huo mgomo.....!!
Mlipowaomba waandike mabango na wakatae kuingia darasani ili malengo ya wanaharakati feki yatimie...masikini wanafunzi waliitikia wito wenu na kuwaamini.................!!
Mlipowahamasisha waimbe kwa nguvu na wakimbie kwa nguvu na wahamasisheni...masikini wanafunzi waliitikia wito wenu na kufanya hivyo...........!!
Sasa wapo vijijini kwao na wameambiwa warudi kwa mashrti kibao...na wengine watashindwa......!!
Kibaya zaidi wale wa Ushirika wameambiwa walete na vyeti vyao vya form 4 na 6 wadahiliwe upya......................!!
Endapo mwanafunzi yeyote yule atapoteza chuo kwa upumbavu wenu viongozi wa wanafunzi........basi damu yake iwe juu yenu..........!!....Laana iwe juu yenu kwasababu sasa wapo kwenye matatizo mpo kimya na hamuwasaidii chochote...ila wao waliwasaidia kutimiza malengo yenu..........!!
HEBU NENDENI KANISANI MTUBU MAKOSA YENU NA MUMUOMBE MUNGU ASIPOTEE HATA MWANAFUNZI MMOJA..SABABU LAANA ITAKUWA JUU YENU!!

WAKATI WA KUIMBA NA KUKIMBIAKIMBIA RAHA SAANA...LAKINI....!!!


Natuma salamu zangu kwa mjiitao wanaharakati popote mlipo....saalam pia kwa wote mliokuwa mnaimba kama sio juhudi zake baba wa taifa....salamu kwa wote mliokuwa mkitumia slogan yenu feki ya eti mpaka kieleweke......!!
ilikuwa raha sana kukimbikimbia around chuo....na ilikuwa raha sana kuimba na kukataa vipindi mkiwa na wenzenu pale chuoni.........!!
Ujinga wenu ni pale mlipokuwa hamjui ni nini na ni nani aliye nyuma ya mgomo wenu feki......!!!
Walewale waliokataa sera..haohao wanajaza fomu ya kuikubali sera..................!!
mama yangu....kweli mmekosa akili ya upambanuzi wa mambo............mlikuwa mnaona raha sana kuimba mkiwa pamoja..ila sasa kila mtu yuko nyumbani kwao na ndipo anapogundua kuwa kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe.....!!
Sasa unahangaika wewe na mama yako kutafuta fwedha ulipe urudi chuoni...........!!Ilikuwa raha sana kuimba na kutoka jasho...ila mtoto wa mwaka wa kwanza na wa pili alipoambiwa rudi nyumbani huku nauli hana mfukoni....ndipo alipokumbuka kuwa kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe....Niliwakuta Ubungo Bus Terminal wakiwa wamebung`aa na mimacho yao hawajui pa kwenda.....!!...Muwe na fikira zinazojitegemea na msiongozwe na hao wanaharakati feki wanaokuwa sponsored na watu fulani.....!!
HAYA ENDELEENI KUJAZA FOMU ILI MRUDISHWE....ILA MKIRUDI KAENI CHINI MUORODHESHE FAIDA NA HASARA MLIZOPATA....!!

Thursday, December 18, 2008

TUTAKUKUMBUKA DAIMA "ODONG ODWAR"

Saalam Wadau,

Ninapolitaja jina la huyo mtu hapo juu ninaamini si geni kwa wanafunzi wengi wa vyuo vikuu na Tanzania kwa ujumla.........!!
Enzi za uwepo wake alikuwa ni mwanafunzi wa sheria katika chuo kikuu cha Dar Es Saalam...na kabla ya kutimuliwa kurudi kwao Uganda alikuwa mwaka wa tatu.............!!

Tutamkumbuka huyu mpiganaji kwa mambo mengi sana...ikiwa ni pamoja na zengwe alizofanyiwa kipindi alichotaka kuwa Rais wa Daruso lakini Serikali na Chuo wakaogopa kwa kudhani kuwa UDSM patachafuka sana kwa migomo na dhambi zao zitatajwa kwa majina.................!!

Pia alikuwa mstari wa mbele katika kuongoza harakati mbalimbali pale mlimani zikiwepo harakati feki na zisizo feki...mfano halisi ni zile harakati za kuifuta 40% ambazo kiasi fulani tulifanikiwa na nyingine ndogondogo lakini kubwa zaidi ni hizi harakati feki za juzi ambazo aliziongoza yeye na ndugu zake kina OWAWA na SILINDE ambazo zilifanya vyuo vya umma vifungwe na wao wapate mabalaa na wengine kwenda kujificha mikoani.

Sitasahau jinsi tulivyimpigania kipindi alichofukuzwa chuo kwa hila kisa tu aligombea Urais na tukagoma mpaka akarudishwa yeye na wenzake na tukamuondoa rais mamluki bwana Pasience........!!

Kwanza namsifia kwa baadhi ya mambo aliyofanya he was a real HERO na kwa mambo mengine machache hayo sitaacha kumponda!!.Lakini intention ya huyu mganda ilikuwa ni nini?..bado ninajiuliza sana!!..na kwa nini alijiingiza katika vyama vya siasa vya nchini wakati yeye si raia??..bado najiuliza sana........!!

NENDA ODONG ODWAR TUTAKUKUMBUKA DAIMA....YOUR FOOTPRINTS ARE STILL THERE AT THE HILL!!

WASALIMIE MARAFIKI WA UGANDA....GOD BLESS YOU IN YOUR FUTURE ENDEVORS!!